Na.Khadija seif, Michuzi TV.

WALINZI shirikishi pamoja na mabaunsa wametunukiwa vyeti baada ya Kumaliza mafunzo yao ya ulinzi shirikishi kupitia Jeshi la Polisi (TPSIS)

Juma Gabriel ni mmoja wa Wakufunzi waliopatiwa mafunzo kutoka jeshi la polisi (TPSIS) nakutambulika kama mmoja wa walinzi shiriki.

Gabriel amesema mafunzo hayo yanawapa wepesi wa kujitambua na kutambulika kisheria tofauti na walinzi ambao jeshi la polisi haliwatambui pamoja na weledi.

"Mafunzo hayo yameweza kutupatia elimu ya ziada ambapo wengi wetu tulikua hatufahamu pamoja na kitambulisho kitakachotusaidia kutambulika mbele ya jamii pindi tuwapo kwenye doria ,"

Amezitaja nafasi ambazo walinzi hao shiriki ufanya ikiwemo walinzi wa makampuni,mlinzi wa mtu maarufu au Kiongozi haya yeye ni mlinzi wa msanii Mbosso kutoka kundi la wasafi.

"Imenipa fursa Sasa niweze kufanya kazi zangu kwa weledi na ufanisi kwani mwanzo tulikua hatujawahi kuwekwa pamoja na kufanya mafunzo Kama hayo,"

Pia ametoa pongezi kwa jeshi la polisi (TPSIS)kuiona fursa kwao kutoa mafunzo hayo kwa baunsa hao ili kuwawezesha kutambulika kwa urahisi na kuhalalisha kazi hiyo Kama kazi nyingine za kulinda mali ya umma na wanajamii pamoja na kupewa mbinu nyingi za kikazi zaidi.

Kwa upande wake Muhitimu wa mfunzo hayo Elias Masoud amesema muda wa mafunzo hayo umekuwa ni wa siku tatu na amewaomba uongozi kuona fursa nyingine kuongeza siku kwa awamu nyingine ili kujifunza zaidi.

"Mafunzo yanatija sana kwa jamii kwani majukumu ya kazi inakua rahisi kwa jeshi la polisi kuwa pamoja na ulinzi shirikishi (Mabaunsa) na kufanya kazi kwa pamoja,"

Pia ametoa ushauri kwa wamiliki wa walinzi shiriki hao kuwapa nafasi kwenda kujifunza mafunzo hayo kwa usalama wa mali zao pamoja na wao wenyewe kwa ujumla.
 Afisa Mnadhimu wa jeshi la polisi ACP.Janeth Magombi akimkabidhi cheti mmoja wa washiriki katika mafunzo ya ulinzi shirikishi kwa walinzi wa makampuni pamoja mabaunsa waliopata mafunzo siku tatu jijini Dar es salaam
Picha ya pamoja ya baadhi ya washiriki waliopatiwa mafunzo ya siku tatu ya weledi kazini na kujitambua kutoka sekta binafsi jeshi la polisi (TPSIS) wakiwa na Afisa Mnadhimu wa jeshi la polisi ACP.Janeth Magombi pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa sekta binafsi ya kutow mafunzo ya ulinzi shirikishi (TPSIS)  Dr. David Rwegoshora

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...