Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe akizungumza katika maadhimisho ya miaka 40 ya Umoja wa posta barani Afrika
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Maria Sasabo akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi katika maadhimisho ya miaka 40 ya Umoja wa Posta Barani Afrika(PAPU)
Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe akisalimiana na mmoja wa maofisa wa polisi alipowasili katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Jijini Arusha
Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi kutoka nchi wanachama wa Umoja wa posta Barani Afrika
Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe akizungumza na viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa posta Barani Afrika katika maadhimisho ya miaka 40
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Dkt. Maria Sasabo akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa nchi wanachama wa Umoja wa posta barani Afrika (PAPU)
Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Aloyce Kamwelwe mmoja wa washiriki wa maadhimisho ya miaka 40 ya Umoja wa posta barani Afrika
Na.Vero Ignatus Arusha.
Madhimisho ya miaka 40 ya umoja wa posta barani Afrika yameadhimishwa leo jijini Arusha ambapo umoja huo ulianzishwa na Muasisi wa Taifa la Tanzania Hayati Mwl.JK.Nyerere pamoja na viongozi wenzake ili waweze kuwa na sauti moja katika umoja wa posta duniani tangia kuanzishwa kwake mwaka 1980.
Aidha viongozi hao waliona Afrika walikuwa hawajaungana na dunia katika mambo mbalimbali hivyo wakaamua kuanzisha umoja wa posta ili waweze kuwa na sauti ya pamoja ili wasikilizwe na umoja wa dunia kwa masuala ya posta.
Akizungumza katika ufunguzi wa maadhimisho hayo Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe amesema kuwa hadi sasa yapo mambo mengi yamekwisha kufanyika katika kuhakikisha kwamba posta inafanya kazi na watanzania kwa karibu zaidi ambapo hadi sasa posta zimekuwa kila wilaya
‘’ Hapo muda kidogpo posta ilikuwa haijafanya vizuri ila awamu ya tano ya dkt magufuli ambaye alifuatilia mambo yote yaliyoanzishwa na na mwanzilishi wan chi hii pamoja na mambo mengine ameuufufua umoja huuna umerudi kwa malengo yaleyale yaliyowekwa na waanzilishi
Kamwelwe amezishauri wanachama wa mashirika ya posta barani Afrika PAPU kuanza kujikita katika kutoa huduma za kifedha haswa kutokana na kuwa na mtandao mkubwa katika nchi hizo
''Afrika ina nchi Zaidi ya 54 katika umoja wa posta zipo nchi 45 ambazo zimesajiunga na umoja huo ambapo makao makuu ya umoja huo yapo Nchini Tanzania jijini Arusha''
Amesema kuwa Januari 18,2020 wataweka jiwe la msingi kwaajili ya kujenga ofisi ya umoja wa posta Tanzania itakayogharimu jumla ya shilingi bilioni 33 za kitanzania,fedha ambazo asilimia 40%zimechangiwa na serikali ya nchiwashirika wa post ana asilimia nyingine 40 zimechangiwa taasisi ya TCRA.
Kwa upande wake katibu mkuu wa PAPU Younouss Djibrine amesema kuwa nchi wanachama wanatakiwa kuboresha matumizi ya mtandao katika kuboresha huduma zao .Hata hivyo alisema kuwa bado kuna matumizi makubwa ya teknolojia ya mawasiliano jambo ambalo linahitajika kuboreshwa zaidi
Kwa upande wake Meneja mkuu wa shirika la posta nchini Mhandisi Hassan Mwang’ombe amesema kuwa upelekaji wa vifurushi kwa wananchi amesema wanaimarisha huduma za posta kwa kuziunganisha pamoja na mtandao TEHAMA (ICT) ili wananchi waweze kupata huduma kwa haraka zaidi
Amewaasa wananchi kutumia huduma za posta kwa sababu wapo wataalam na vifaa kwa ajili ya kufanyia ukaguzi mizigo yote kabla ya kusafirishwa (scanner) hivyo mwananchi anapopata kwa njia ya huduma ya posta mzigo unasafiri ukiwa salama unakaguliwa
''Serikali haitaki mabasi yasafirishe vifurushi kwasababu havikaguliwi na haijulikani wamebeba mizigo ya ania gani,wakati mwingine wanabeba hata madawa ya kulevya ,mihadharati hata mizigo hatarishi kwa binadamu’’alisema
Amesema hadi sasa posta imehakikisha kuwa kila Kijiji kina namba na kinatambulika sambamba na anwani za makazi ili kuwatambua watanzania na kumfikia mteja popote alipo bila shaka kwa sababu kama mwananchi hupati huduma kama unavyotaka ni tatizo
Amesema kuwa kutokana na utandawazi kuingia wao kama posta wameugeuza kuwa fursa ndiyo maana kwa sasa posta wanajitahidi kujikita zaidi ili kumfikia mtanzania na kuhakikisha anapata habari za vifurushi vyake popote walipo
Ameeleza kuwa huduma nyingi zitakwenda vijijini kuwafuata wananchi ili wasipate tabu ya kutembea kwenda mbali kwasababu hayo ndiyo malengo ya maadhimisho ya miaka 40 ambayo yamekubaliwa na nchi zote za umoja wa Afrika pamoja na wapenda maendeleo wote duniani
Mwang'ombe amesema kuwa hadi sasa kwenye ofisi za kata zipo ofisi za posta katika utoaji wa huduma wananchi wanapokea huduma kwa njia ya mtandao kwasababu watananchi wanatumia huduma za vifurushi,barua ,fedha na uduma zingine
''Japo kuwa yapo maendeleo mbalimbali ya kiteknolojia lakini bado tunasema kuna umuhimu wa bidhaa kusafiri kutoka eneo moja kwenda nyingine kwani wananchi waanagiza bidhaa mbalimbali kutoka kona zote za dunia''
Maandhimisho hayo ambayo yanakwenda sambamba na uwekaji wa jiwe la msingi wa jengo la makao makuu ya umoja wa posta Afrika sanjari na harambee ya kuchangia ujenzi huo ambao utafanyika kesho jijini Arusha.
Shirika la posta Tanzania lilianza mwaka 1994 ambapo kabla ya hapo ilikuwa imeunganishwa na shirika la posta na simu umoja wa umoja wa posta Afrika ulianzishwa mwaka januari 1980.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...