RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akikagua gwaride Maalum
la Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika
katika Uwanja wa Amaan Zanzibar.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza vla Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasalimia Wananchi
wakati wa Maadhimisho ya Sherehe za Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar
yaliyofanyika katika Uwanja wa Amaan Zanzibar
Mgeni rasmi,Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein akisalimiana na Rais Mstaafu wa Zanzibar wa awamu ya sita Dk. Amani Abeid Karume alipowasili jukwaa kuu,katika Maadhimisho
ya Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofanyika
katika Uwanja wa Amaan Zanzibar.Pichani kati anaeshuhudia ni Rais
Mstaafu wa awamu ya nne wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya
Mrisho Kikwete.

VIJANA wa Maandamano Maalum ya
kuadhimisha Miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar wakiwa na Picha za Waasisi
wa Mapinduzi, wakati wa hafla hiy0 iliofanyika Uwanja wa Amaan
Zanzibar.

Vijana wa Chama cha mapinduzi
wakipita mbele ya Mgeni Rasmi ikiwa ni Ishara ya kutoa heshima katika
maandamano ya maadhimisho ya ya Miaka 56 ya Mapinduzi yaliofanyika Aman
mjini Zanzibar.

WANACHAMA wa Chama cha CUF
wakishiriki katika Maandamano ya kuadhimisha sherehe za Miaka 56 ya
Mapinduzi Zanzibar zilizofanyika Uwanja wa Amaan Zanzibar

VIJANA wa payunia wakitowa salamu
ya heshima kwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi
Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein wakati wa maandamano ya Miaka 56 ya Mapinduzi
ya Zanzibar.

Vikosi vya Jeshi la Ulinzi na Usalama Vikipita mbele ya Mgeni Rasmi katika Maadhimisho ya miaka 56 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar
Balozi Seif Ali Idi akitoa hotuba ya Makaribisho kwa Mgeni Rasmi katika
kilele cha Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi yaliofanyika Aman mjini
Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Dk Ali Mohamed Shein akitoa hotuba ya kilele cha
Maadhimisho ya Miaka 56 ya Mapinduzi yaliofanyika Aman mjini Zanzibar.PICHA NA IKULU PAMOJA NA YUSSUF SIMAI/MAELEZO ZANZIBAR.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...