
Hatua hiyo inatokana na
mwitikio mdogo wa waliothibitisha kushiriki, hivyo kufanya maandalizi mengine
ya mkutano huo kushindwa kufanyika vizuri.
Kwa mazingira hayo mwisho
ya kuthibitisha kushiriki itakuwa Jumatatu Januari 13 mwaka huu, na mkutano huo
sasa utafanyika Jumapili Januari 19 na hakutakuwa na muda wa ziada kwa watakaoshindwa
kuthibitisha.
Lengo la mkutano huo ni kujadili masuala mbalimbali ya chama,
ambapo pia utapokea taarifa kutoka Kamati ya Marekebisho ya Katiba iliyoundwa
na Baraza la Michezo la Taifa (BMT) na pia utapokea mapendekezo kutoka Kamati
ya Utendaji ya TASWA inayomaliza muda
wake.
Watakaohudhuria Mkutano Mkuu Maalum ni wanachama wote walio katika leja baada ya kushiriki uchaguzi wowote wa TASWA kuanzia mwaka 2004, 2007, 2010, 2014 na wanachama wapya wote walioingia kuanzia mwaka 2015 hadi Juni mwaka jana.
Kwa
mazingira hayo ili mkutano ufanyike kwa ufanisi ni vyema yeyote mwenye nia ya kushiriki
athibitishe kwa maandishi akitaja jina lake na chombo na kutuma kwa email: taswatz@yahoo.com au mgosius@yahoo.com au machagift@gmail.com, ili taratibu nyingine ziendele.
Nawasilisha,
Amir Mhando
Katibu Mkuu TASWA
10/01/2020
10/01/2020
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...