WAZIRI
 MKUU Kassim Majaliwa amewataka Watanzania washirikiane katika kuulinda 
na kuutetea Muungano wa Tanzania pamoja na Mapinduzi Matukufu ya 
Zanzibar na kamwe wasiruhusu watu kuingiza sumu ya kutaka kuwagawa.
Ameyasema
 hayo jana (Ijumaa, Januari 17, 2020) wakati akizungumza kwa nyakati 
tofauti na wananchi katika mikutano iliyofanyika wilaya ya Kati na 
wilaya ya Kusini alipokuwa katika ziara yake ya kikazi mkoa wa Kusini 
Unguja.
“Watanzania
 tusikubali mtu yeyote kutugawa kwa sababu sisi undugu wetu ni wa damu, 
hivyo ni vema tukaendelea kuudumisha muungano wetu tusiruhusu watu 
kuingiza sumu ya kutaka kutugawa kwani watu hao hawana tija.”
Waziri
 Mkuu ambaye awali alikagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa maabara 
ya sayansi katika shule ya sekondari ya Bwejuu, mradi wa kilimo cha 
kisasa Jozani na kuzindua jengo la mama na mtoto Bambi. Amesema hayo 
yote ni matunda ya muungano hivyo, hawana budi kuendelea kuudumisha.
Akikagua
 maendeleo ya ujenzi wa maabara ya sayansi katika shule ya sekondari ya 
Bwejuu, Waziri Mkuu ametoa muda wa miezi mitatu kwa mkandarasi 
anayejenga maabara hiyo awe amekamilisha kazi hiyo.
Pia, Waziri Mkuu alimwagiza Mkuu
 wa Mkoa wa Kusini Unguja, Bw. Ayoub Mohammed Mahmoud ahakikishe 
watumishi wanatenga muda wa siku nne kwa wiki kwa ajili ya kwenda 
kuwahudumia wananchi katika maeneo yao hususan ya vijiji. 
Vilevile,
 Waziri Mkuu aliagiza Maafisa kilimo wahamishiwe vijijini ili waweze 
kuwasimamia vizuri wakulima ikiwa ni pamoja na kuwashauri namna bora ya 
kulima kwa kufuata kanuni na matumizi mazuri ya pembejeo.
Kadhalika,
 Waziri Mkuu alisisitiza umuhimu wa kutoa huduma kwa wananchi wote bila 
ya kujali dini, kabila, rangi wala itikadi za chama kwa kuwa lengo la 
Serikali ni kuhakikisha wananchi wote wananufaika na kuhudumiwa bila ya 
kubaguliwa kwa namna yoyote.
Awali,
 viongozi mbalimbali wa vyama vya upinzani wakiwemo wa vyama vya CUF, 
NRA, UPDP, NSSR-MAGEUZI waliipongeza Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa
 Tanzania (SMT) pamoja na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kwa 
kuimarisha huduma za kijamii.
Viongozi
 hao walisema kuwa wapo tayari kushirikiana na Rais Dkt. John Pombe 
Magufuli pamoja na Rais Dkt. Ali Mohammed Shein kwa sababu viongozi hao 
wanafanya kazi kubwa na nzuri ya kuwahudumia wananchi.
“Maendeleo
 hayana chama naunga mkono jitihada zinazofanywa na SMT na SMZ na 
nimefurahia ziara ya Waziri Mkuu hapa kisiwani Unguja na ninamuunga 
mkono Rais Dkt. Magufuli tumepata maendeleo ambayo hatukuyatarajia,” 
alisema Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa NRA Bw. Khamis Faki katika mkutano
 wa hadhara uliofanyika Shehia ya Bambi.


 
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...