Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage akizungumza na waandishi wa habari juu ya kufanyika kwa zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kwa mikoa ya Morogoro na Tanga.
NA FARIDA SAIDY, MOROGORO
Zoezi la uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura linatarajiwa kufanyika kwa
siku saba kuanzia januari 23 hadi 29, 2020 katika mikoa ya Morogoro na
Tanga.
Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi Mhe Jaji
Mstaafu Semistocles Kaijage Katika mkutano wa tume na wadau wa
uchaguzi mkoa wa Morogoro uliofanyika januari 15, 2020 katika
ukumbi wa mkuu wa mkoa.
Jaji Kaijage amesema mpaka sasa tume imeshakamilisha maandalizi
kwaajili zoezi hilo kwa mikoa ya morogoro na Tanga na kwamba
uboreshaji wa daftari la wapiga kura tayari ulikwisha anza kwa mikoa 25
ya Tanzania bara na zanzibar tangu kuanzishwa kwake july 18,2019
Mkoani kilimanjaro.
Amefafanua kuwa miongoni mwa maboresho yanatarajiwa kufanyika ni
pamoja na kufanyika marekebisho kwa mwananchi ambaye
alijiandikisha katika kituo kingine na amehama eneo hilo kwamba
taarifa zake zitaweza kurekebishwa kulingana na eneo alipo.
Mwenyekiti mh. jaji kaijage ameeleza kuwa uboreshaji wa safari hii
hauhusishi wapiga kura wote walioandikishwa 2015, bali uboreshaji huu
utawahusu wapiga kura wapya ambao wametimiza au watatimiza umri
wa miaka 18 mwaka huu 2020 siku ya uchaguzi mkuu.
Katika upande wa elimu ya mpiga kura ameeleza kuwa inaendelea
kutolewa kupitia vyombo ya habari, gari la matangazo la tume ya
uchaguzi ambalo limekua likipita maeneo baadhi ya maeneo, kwenye
mikusanyiko ya watu kama vile sokoni na matamasha pia mitandao ya
kijamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...