Zoezi la Uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura katika Wilaya ya Tandahimba limeanza rasmi huku wananchi wakionekana kuhamasika na zoezi Hilo kwa kujitokeza kwa wingi katika maeneo tofauti Wilayani hapa
Akizungumza katika kituo Cha Uandikishaji Nambahu Afisa Mwandikishaji daftari la kudumu la wapiga kura Jimbo la Tandahimba Said Msomoka alieleza kuwa amefarijika kuona wananchi wamehamasika na zoezi Hilo
Aidha aliwataka wananchi wajitokeze kwa wingi ili kujiandikisha na kuboresha taarifa zao katika daftari la kudumu la wapiga kura
Zoezi la kuboresha daftari la kudumu la wapiga kura Wilayani Tandahimba limeanza rasmi na linatarajia kumalizika jumapili wiki hii.
Mwananchi akiwa anafurahi kupata kadi yake ya kupiga kura
Wanachi wamejitokeza kwa ajili ya kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura
Wananchi wakisubiri kujiandikisha
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...