Rais wa Marekani Donald Trump, ametangaza kuweka zuio kwa raia wa nchi za Ulaya kuingia nchini Marekani ili kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona.

Katika hotuba yake kwa njia ya Televisheni siku ya Jumatano, amesema safari zote za kutoka Ulaya zitazuiwa kwa siku 30 zijazo.

Lakini amesema ''hatua kali lakini zilizo na umuhimu'' hazitaihusisha Uingereza, ambayo ina visa 460 vya virusi vilivyothibitishwa.

Kuna visa 1,135 vilivyothibitishwa nchini Marekani na watu 38 wameripotiwa kupoteza maisha.

''Kuzuia visa vipya kuingia Marekani, tutaahirisha safari zote kutoka Ulaya,'' Trump alieleza.

''Hatua hii itaanza kutekelezwa kuanzia usiku wa siku ya Ijumaa''. Aliongeza.

Tump amesema Umoja wa Ulaya ''umeshindwa kuchukua hatua za tahadhari kama hizo'' zilizoanzishwa na Marekani.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...