Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi anawataarifu  Maafisa Habari na Mawasiliano Serikalini pamoja na wadau wengine kuwa Kikao Kazi kilichotarajiwa kufanyika tarehe 9 hadi 13 Machi 2020, Jijini Mbeya kimeahirishwa.

Kikao kazi hicho ambacho hufanyika kila mwaka ili kuwajengea uwezo Maafisa Habari na Mawasiliano wa Serikali namna ya kutangaza shughuli za Serikali na kuhakikisha,  Idara na Vitengo vya Mawasiliano na Uhusiano Serikalini vinaimarishwa ili kuendana na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano na Teknolojia mpya ya Habari na Mawasiliano katika kuwahudumia wananchi.

Aidha, Maafisa hao wametakiwa kuendelea  kutekeleza majukumu yao katika maeneo  ya kazi kwa kutangaza utekelezaji wa Serikali ili wananchi waweze kupata taarifa muhimu za Serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...