SHIRIKA la ndege la Emirates limeanzisha sera mpya za nyongeza  zitakazowapa uhuru wateja wao katika kupata huduma za usafiri.

Shirika hilo limekuja na sera hizo kwa kuwakarimu wateja kwa kutoa machaguo zaidi katika kupanga mipango ya safari zao.

Imeelezwa kuwa shirika hilo limewapa uwezo wateja kubadili tarehe za safari zao bila makato kuanzia Machi 7 hadi 31 mwaka huu.

Pia imeelezwa kuwa wateja wa Emirates wanaweza kubadilisha ratiba za safari zao na hiyo ni kutokana na mlipuko wa virusi vya Corona (Covid 19) na wateja watakuwa huru kubadili tarehe za kusafiri ndani ya miezi 11 kwa daraja lilelile bila makato yoyote na sera hiyo mpya inahusisha maeneo yote ambayo yana mtandao wa Shirika hilo la Emirates.

Afisa Mkuu wa biashara wa Emirates Adnan Kazim amesema kuwa,
"Tunapenda wateja watu wajisikie wakiungwa mkono kikamilifu wakati wa kupanga mipango yao ya kusafiri kwa kulipa nauli zao na kufanya mabadiliko bila ada ya ziada" Ameeleza.

Amesema kuwa ikiwa wateja watabadili tarehe za kusafiri wataendelea kutafuta njia faafu, rahisi na zitakazowaridhisha wateja.

Pia imeelezwa kuwa shirika hilo lipo makini katika katika kuchukua tahadhari kufuatia mlipuko wa virusi vya Covid 19 na hiyo ni pamoja na kuweka mchakato wakusafisha ndege zote kwa kemikali Kali zilizoidhinishwa, na kuelezwa kuwa ikiwa itaarifiwa kuwa na kesi yoyote iliyothibitishwa hatua madhubuti zitachukuliwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...