Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Klabu
ya Simba kwa kushirikiana na Taasisi ya Mo Dewji imehitimisha zoezi la
ugawaji wa Barakoa kwa wakazi wa maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es
Salaam.
Zoezi
hilo limehitimishwa kwa watendaji wa taasisi hiyo kukabidhi barakoa kwa
ajili ya kujilinda na homa kali ya Mapafu (COVID-19) inayosababishwa na
virusi vya corona.
Ikiwa
ni siku ya tatu toka kuanza kwa ugawaji wa barakoa hizo, wananchi
wamefurahia zoezi hilo la kuwakumbuka wananchi hususani wale ambao
hawana uwezo wa kununua wenye kipato cha chini.
Barakoa
zimekuwa zikishauriwa kutumiwa kama njia ya kupunguza uwezekano wa
kusambaza virusi hivo pale ambapo mtu atakua ana kohoa ama kupiga chafya
pamoja na kupunguza umbali ambao maji maji hayo yanaweza kuruka.
Barakoa
hizo zimetengenezwa hapa nchini na kampuni ya Mohammed Enterprises
Tanzania Limited kwa kutumia pamba inayolimwa hapa nchini. Barakoa hizi
ni imara na hivo kuruhusu uwezekano wa kutumika zaidi ya mara moja baada
ya kufuliwa na kupigwa pasi.
Klabu
ya Simba imeendelea kuchukua tahadhari kwa kuwalinda wachezaji wake na
zoezi hili limekua na lengo la kuwakumbuka wananchi na mashabiki wake
pamoja na kuwasihi waendelee kufuata hatua zinazoelekezwa.
Taasisi
ya Mo Dewji imejitolea barakoa 25,000 kwa Mkoa wa Dar es Salaam ikiwa
ni mwendelezo wa kurudisha kwa jamii kwa kuangalia namna bora ambazo
inaweza kusaidia katika mapambano dhidi virusi vya corona. Hususani kwa
wananchi wa kawaida kuweza kujilinda na kupambana na virusi hivo.
Ugawaji
wa barakoa hizo umefanyika katika masoko na vituo vya boda boda mbali
mbali jijini Dar es Salaam ikiwemo maeneo ya Kivukoni, Kariakooo,
Tandale, Manzese, Buguruni, Makumbusho, Mabibo, Temeke, Mbagala,
Msasani, Kimara, Mbezi na Tegeta.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...