Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
Shirika
la ndege la Precision Air wamezindua safari za ndege ya mizigo kutokea
Tanzania na kuelekea Hahaya katika Visiwa vya Comoros wakipeleka bidhaa
mbalimbali.
Safari hizo zimeanza rasmi siku ya Jumamosi kutokana na mabadiliko katika soko na nchi nyingi kufunga mipaka yao.
Akitoa
taarifa hiyo, Meneja Masoko na Mawasiliano amesema wamebadilisha moja
ya ndege zao aina ya ATR72-500 kuwa ndege ya mizigo, na safari ya kwanza
ilikuwa ni siku ya Jumamosi.
Amesema,
kutokana na mabadiliko katika soko safari yao ya kwanza ya mizigo
kuelekea Hahaya waliweza kusafirisha madawa pamoja na mbogamboga.
Mremi
ameeleza kuwa Kupitia safari hiyo ya kwanza pia wamezindua rasmi safari
za mizigo ambapo zitakuwa zikifanyika kila Jumatano kuelekea Hahaya.
Mremi amesema, ndege hyo ya ATR72-500 ina uwezo wa kubeba tani 5.5 kwa wakati mmoja na itapeleka mahitaji muhimu kila wiki.
Aidha, safari za ndani na kikanda zitaendelea kulingana na mahitaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...