Na Amiri Kilagalila, Njombe.

Edwin Swale aliyewahi kuwa mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Njombe,ameshinda kura za maoni katika mkutano mkuu wa jimbo la Lupembe mkoani Njombe kwa kupata kura 138 kati ya kura 421 kuwa mgombea wa ubunge Jimbo hilo kupitia Chama cha Mapinduzi CCM huku Jorum Hongoli aliyekuwa akitetea nafasi yake akipata kura 61.

Edwin Enosy Swale (wakili) alihamia Chama cha Mapinduzi Octoba 2019.
Mkutano wa kura za maoni umefanyika mapema hii Leo katika ukumbi wa Turbo mjini Njombe kwa kuwapigia kura wagombea 19 waliojitokeza kuwania nafasi hiyo.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...