Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akiongea na wananchi wa kijiji cha Rungemba wakati wa ziara ya kukagua miradi pamoja na kusikiliza kero za wananchi
Stephen Kalinga akiwa kwenye gari ya polisi baada ya mkuu wa mkoa kuamuru akamatwe kwa kosa la kuongea uongo kwenye mkutano wa hadhara
Stephen Kalinga na mwenzake wakiwa kwenye gari ya polisi baada ya mkuu wa mkoa kuamuru wakamatwe kwa kosa la kuongea uongo kwenye mkutano wa hadhara

Na Fredy-Mgunda,Iringa.


Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi ameamuru kukamatwa kwa mwenyekiti wa bodi ya maji ya kijiji cha lungemba wilayani mufindi Stephen Kalinga kwa kosa la kuwamchonganishi baina ya serikali na wananchi huku akiahidi kuchangia mifuko 100ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa wodi la akinamama.

 Akizungumzawakati wa ziara ya kukagua miradi halmashauri ya Mji wa Mafinga katika zahatiya kijiji cha Rungemba, mkuu wa mkoa alibaini kuwepo kwa tuhuma ambazo hazinaukweli wote.

Akisikilizakero za wananchi wa kijiji hicho,mkuu wa mkoa alipokea barua kutoka kwamwananchi iliyokuwa inatuhuma kwa baadhi ya viongozi wa kijiji hicho na kuanzakuzitafutia majibu kwa viongozi waliokuwa wametajwa.

 Baada yakubaini kuwa ndugu Stephen Kalinga alitoa tuhuma ambazo zilikuwa hazina ukwelikwa baadhi ya viongozi wa kijiji hicho ndipo alipoamuru kukamatwa kwa mwananchihuyo ili aende kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi.

Lakinimkuu wa mkoa Ally Hapi alimvua cheo cha kuwa mwenyekiti wa kamati ya maji yakijiji hicho na kuteua kiongozi mwingine wa muda hadi pale mkutano wa kijijiutakapopitisha jina la kiongozi mpya.


Hata hivyoviongozi wa kijiji kijiji hicho na wananchi walimuunga mkono mkuu wa mkoa wa IringaAlly Hapi kwa uamuzi wa kumvua vyeo bwana Stephen Kalinga kwa kuongea uongoambao ulitaka kuvuruga amani ya wananchi wa kijiji cha Rungemba.

 AidhaHapi alitoa ahadi ya kuwa kutoa mifuko mia moja ya saruji kwa ajili ya ujenziwa jingo la hodi ya akina mama ikiwa ni kuunga mkono juhudi ambazo zinafanywana wananchi wa kijiji cha Rungemba kuleta maendeleo na kuboresha sekta ya afya.

Hapialiongeza kwa kusema kuwa wananchi watakiwa kuendelea kujitolea katika shughuliza kimaendeleo kama kuiboresha zahanati hiyo hadi kufikia hadhi ya kuwa kituocha afya lengo kuu likiwa ni kuendelea kuboresha sekta ya afya.

 “Naomba wananchi wengine wa moa wa Iringa kuiga mfano wa wananchi wa kijiji cha Rungemba kwajitihada zao wanazozifanya kuhakikisha wanafanya shughuli za kimaendeleokijijini kwao” alisema Hapi  

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...