Msimamizi wa 
Uchaguzi wa Jimbo la Nzega Mjini Philemon Magesa alifungua jana mafunzo 
ya siku tatu ya wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata.
 
 
Hakimu Mkazi 
Mwandamizi Mfawidhi wilaya ya Nzega Glays Barthy akitoa maelekezo ya 
kuzingatia jana kwa Wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata za Jimbo la Nzega
 Mjini.
 
 
Hakimu Mkazi 
Mwandamizi Mfawidhi wa Wilaya ya Nzega Glays Barthy awaapisha wasimamizi
 wasaidizi ngazi ya Kata za Jimbo la Nzega Mjini.
 ……………………………………………………………………………..
NA TIGANYA VINCENT
MSIMAMIZI wa 
Uchaguzi wa Jimbo la Nzega Mjini Philemon Magesa amewataka Wasimamizi 
wasaidizi ngazi ya Kata kuepuka ushabaki  wa aina yoyote wa kisiasa 
katika utekelezaji wa majukumu yao ili kutosababisha vurugu wakati zoezi
 la uchaguzi mkuu ujao.
Alitoa kauli 
hiyo jana wakati akifungua mafunzo ya Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi 
Mkuu ujao kutoka Kata 20 za Halmashauri hiyo.
Magesa 
alisema  ili Wasimamizi wasaidizi wawe salama katika zoezi hilo ni vema 
wakazingatia Katiba , Sheria na Kanuni zinasimamia zoezi zima la 
uchaguzi.
Alisema hali 
hiyo itasaidia kuufanya uchaguzi kuwa mzuri, wenye ufanisi na hivyo 
kuondoa kabisa malalamiko au vurugu wakati wote wa mchakato wa uchaguzi.
Aidha Magesa 
aliongeza kuwa katika utekelezaji wa majukumu yao ni muhimu 
wakavishirikisha vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi katika 
masuala ambayo wanastahili kushirikishwa.
Naye Hakimu 
Mkazi Mwandamizi Mfawidhi Glays Barthy walioteuliwa na Ttume ya Taifa ya
 Uchaguzi(NEC) ambao ni wanachama wa vyama vya siasa kuhakikisha 
wanajitoa katika vyama vyao ili kuweza kusimamizia zoezi kwa umakini.
Aliwataka 
wasimamizi wasadizi hao kuwa makini na watu wa karibu nao kwa kujiepusha
 kutoa maoni ambayo yanaweza kusababisha uvunjifu wa sheria za uchaguzi 
na kanuni zake.
“Muwe makini na
 ma group mnayo socialize kwa kuepuka kutoa maoni ambayo nanaweza 
kusababisha kuonekana unashabikia upande fulani na kusababisha vurugu” 
alionya.
Alisema katika 
kipindi chote cha zoezi la uchaguzi wanapaswa kujizuia kupenda 
kujadiliana na makundi mbalimbali nyakati zote za shughuli za uchaguzi.
“Tunajua baadhi
 yenu mna kazi za vyama vya siasa …baada ya kiapo hiki mnatakiwa kujitoa
 kabisa kuzungumzia mambo ya vyama vyenu ili muweze kuwatendea haki hata
 wote…na wale wenye ushabiki wa ndani ni vema wakaauacha ili waweze 
kutekeza majukumu yao kwa mujibu Katiba, Sheria na kanuni zinazosimamia 
uchaguzi” alisisitiza.


 

Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...