Na Stanslaus Makendi, Mahakama Kuu Dodoma

Mahakama ya Tanzania inatekeleza miradi mbalimbali ya ukarabati na ujenzi wa Mahakama nchini kwa lengo la kuboresha miundombinu yake ili kuwa na mazingira wezeshi ya utaoji wa huduma ya utoaji haki kwa ujumla.


Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa Mikoa kadhaa nchini ambapo miradi mikubwa ya ujenzi wa Mahakama inaendelea. Kwa mwaka wa fedha 2020/2021 Mahakama ya Tanzania inatekeleza jumla ya miradi mitano ya ujenzi wa Mahakama katika Mkoa huo; ikiwemo ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama, Kituo Jumuishi ya Utoaji haki (Intergrated Justice Centre), Mahakama za Wilaya Chemba na Bahi na Mahakama ya Mwanzo Kibaigwa.


Aidha, hatua ya maboresho ya miundombinu ya majengo ya Mahakama nchini inalenga pia kusogeza huduma za haki karibu zaidi na wananchi ili kumuwezesha mwananchi kupata huduma kwa haraka kwa kupunguza umbali na gharama katika kutafuta huduma ya haki. 

Pichani ni picha za miradi ya ujenzi inayoendelea jijini Dodoma.


















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...