Na Leandra Gabriel, Michuzi TV
KAMPUNI ya mafuta ya Total, ambayo ndio kampuni inayoongoza katika sekta uuzaji na usambazaji wa mafuta na vilainishi nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 50, wamehimizwa kutumia vilainishi vyenye ubora ili injini za magari yao zidumu kwa muda mrefu.
Wito huo, umetoleo leo na Mkurugenzi Mkuu wa Total Tanzania Jean-Francois Schoepp wakati wa ziara maalum ya wateja wakubwa wa vilanishi vya magari vya Total, kutembelea kiwanda cha vilanishi cha Total, ili kujionea namna vilainishi hivyo vinavyotengenezwa ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja ya Total, inayoendelea kwa wiki hii.
Jean-Francois Schoepp, amesema, injini za magari zinachakaa upesi na kuchoka mapema, kutokana na madereva kutumia vilainishi vyenye ubora hafifu, na kuwashauri kutumia vilainishi vyenye ubora wa juu kutoka Total, ambavyo hupunguza pia muda wa kufanya marekebisho ya mara kwa mara.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa kitengo maalumu cha vilainishi wa Total, Anam Mwemutsi amesema kampuni hiyo imetenga wiki ya huduma kwa wateja ili kuona huduma wanazozipata pamoja na kubaini changamoto zao na kuzitatua.
Amesema kuwa Kampuni hiyo imekuwa ikizingatia utoaji wa huduma kwa viwango vya kimataifa kwa wauzaji, wasambazaji na watumiaji wa mwisho wa mafuta na bidhaa nyingine vikiwemo vilainishi.
Aidha ameeleza kuwa katika maadhimisho ya wiki ya wateja wafanyakazi hutembelea vituo vya kutolea huduma na kuona namna wateja wanavyopata huduma na katika siku ya leo wateja wamepata fursa ya kutembelea kiwanda cha Total ambacho hutengeneza bidhaa mbalimbali ikiwemo vilainishi.
Mmoja ya wateja waliotembelea kiwanda hicho, Mhandisi. Honeywick Kalenge kutoka Tanga Cement amesema kuwa bidhaa za Total ni bora hasa katika mazingira ya Tanzania kwa kuwa watumiaji wa bidhaa hizo huepuka matengenezo ya mara kwa mara.
Total ni Kampuni ya nne kwa ukubwa duniani na ya kwanza kwa ukubwa barani Afrika na Tanzania ambako ina vituo vya mafuta vipatavyo mia moja, kiwanda cha kuzalisha vilainishi na ipo mbioni kutekeleza mradi wa ujenzi wa mradi mkubwa wa bomba la mafuta kutoka Tanzania hadi Uganda na wanasherekea zaidi ya miaka 50 nchini Tanzania kwa mafanikio lukuki ikiwemo kuwafikia wateja wengi zaidi na kutoa huduma bora.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...