*NHIF yaendelea kutoa elimu umuhimu wa wananchi kuwa na Bima ya Afya.

Na Ripota Wetu,Michuzi TV

Wananchi wamesema utaratibu  wa upimaji wa afya ufanyike Mara kwa mara kwa kuwa na huduma za pamoja kwani kutasaidia wananchi kujua afya zao.

Wamesema katika Maadhimisho ya Wiki ya Magonjwa yasiyoambukiza  ni changamoto ya makundi mbalimbali katika afya ikilinganishwa na miaka nyuma iliyopita.

Akizungumza na Michuzi Blog mwanachi Joseph Marco amesema kuwa kwa sasa makundi ya vijana yako kwenye changamoto ya Magonjwa yasiyoambukiza kutokana na ulaji usiozingatia,Lishe pamoja na kutofanya mazoezi.

Amesema changamoto nyongine ni tatizo la macho huku akisema watu wanamatatizo ya kuona na foleni imekuwa kuwa kubwa.

Nae mwanaisha Abeid amesema kuwa serikali imeweka utaratibu mzuri wa kuadhimisha na kuweka huduma zote za upimaji wa afya.

Afisa Udhibiti Ubora wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Dkt.Baraka Nathael akitoa elimu kuhusiana na Mfuko huo na umuhimu wa wananchi kuwa na Bima ya Afya ya kuweza kumfanya mwananchi kuwa na uhakika wa afya yake wakati wa utoaji huduma kwa wananchi katika Maadhimisho ya Wiki ya Magonjwa yasiyoambukiza yanayoendeleo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.

Wananchi wakipata huduma ya upimaji wa afya na ushauri katika Maadhimisho ya Wiki ya Magonjwa yasiyoambukiza yanayoendeleaa katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Wananchi wakiwa katika gari wakisubiri kufanya vipimo katika gari hilo katika Maadhimisho ya Wiki ya Magonjwa yasiyoambukiza yanayoendeleaa katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...