Na Woinde Shizza , KILIMANJARO
JESHI la Polisi Mkoani Kilimanjaro limetakiwa kufanya uchunguzi wa kina Mara
baada ya kijana, Alexi Alfred Minja mwenye umri wa mika 29 mkazi wa
Marangu Magharibi kijiji cha malambu Mkoani Kilimanjaro kuuawa kikatili
kwa madai ya kuiba Mahindi kwenye shamba la Jirani yake Akizungumza
msemaji wa familia ya Minja kuhusu kuawa kwa mwanae Agustino Thadey
Minja anasema kwamba Marehemu alipigwa na wananchi kwa kutumia magogo
makubwa kumpiga kichwani na kumsababishia kuvuja damu nyingi eneo la
kichwa na kupoteza maisha
Minja
amelezea kwamba mwanae huyu alikuwa hana tabia ya wizi ila kinacho
onekana ni chuki na wivu wa maendeleo ndio kilicho sababisha kijana wake
kupoteza maisha na sio kweli kwamba ameiba mahindi kwani kijijini hapo
Marangu Magharibi wanamiliki shamba kubwa lenye mahindi
Ndugu
zangu waandishi kiukweli tumefika hapa nyumbani nakukuta ndugu yetu
tayari ameisha uawa na watu wasiojulikana hivyo tunaliomba jeshi la
Polisi kufanya uchunguzi kuweza kubaini ninani walio husika na mauaji ya
mwanae kwani mpaka sasa ni siku ya nne mwili uko hospital na hatujui ni
lini tutamzika maana mpaka sasa mwili haujafanyiwa uchunguzi wowote
alisema baba mkubwa wa marehemu Agustino Minja
Alisema
wanacho omba kwa jeshi la Polisi ni kukamatwa kwa watuhumiwa kwani
wanatamba mtaani kufanya mauaji na hakuna wa kuweza kuwafanya lolote
hivyo sheria ichukue mkondo wake wabainike wahalifu na kufikishwa katika
mikono ya sheria.
Naye
Shangazi yake marehemu aliyejitambulisha kwa jina la Magret Thadey Minja
alisema alipigiwa simu akiwa Mkoani morogoro na kupewa taarifa kwamba
Shangazi yake ameuawa kikatili kwa kupigwa na watu Wa sio julikana kwa
madai ya kuiba mahindi
Shangazi
Magret alieleza kwamba hata kama kulikuwepo na wizi kusingetakiwa
kujichukilia sheria mkononi kulipaswa marehemu apelekwe Polisi pamoja na
kidhibiti cha wizi wa mahindi na kufunguliwa mashtaka na sio kupigwa
kwa muda wa Masaa saba bila kupumzishwa hadi kufariki dunia
Alisema kwamba Watuhumiwa walifanya tukio hilo kinyama kwani hakuna mtu
yoyote aliyeshuhudia mauaji hayo hivyo inawezekana ameawa na watu ambao pia ni majambazi na sio watu wasiofahamika
Baadhi
ya majirani walisema walisikia kelele zikipigwa nje kwa muda mrefu na
kujua kwamba ni ugomvi wa vijana wa kawaida tu lakini baadae walisikia
zimezidi na kutoka nje na kukuta ni Alexi amepigwa na walipo muliza
alijibu kuna watu wamenivamia wamenipiga na kuondoka baada ya muda
alifariki dunia
Kaimu
Kamanda wa jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro Ronald Makona
amethibitisha kuwepo kwa tukio hilo na mpaka Sasa baadhi ya watu
wasiopungua watatu wanashikiliwa kwa mahojiano na upelelezi
utakapokamilika watafikishwa mahakamani huku akiitaka familia hiyo kuwa
wavumilivu katika kipindi Cha uchunguzi wa tukio hilo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...