NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA

HALMASHAURI ya Mji Kibaha ,mkoani Pwani, inatarajia kukusanya kiasi cha sh.bilioni 3.9 ya mapato kwa mwaka wa fedha 2020/2021.

Katibu tawala wilaya ya Kibaha Sozi Ngate ambaye alikuwa mgeni rasmi wakati wa kuapishwa madiwani wa Halmashauri ya mji huo, alisema makusanyo ya mwaka 2019/2020 ni bilioni 3.2 ambapo kwa sasa imefikia asilimia 86.

Kwa hatua hiyo ,alieleza ili kufikia malengo ,Halmashauri kwa kushirikiana na madiwani wanapaswa kubuni vyanzo vipya vya mapato.

"Kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tunapaswa kuhakikisha tunakusanya mapato kupitia vyanzo vyetu mbalimbali ambapo makusanyo ya mwaka 2019/2020 ni bilioni 3.2 ambapo kwa sasa imefikia asilimia 86," alisema Ngate.

Alibainisha, makusanyo ndiyo uti wa mgongo wa Halmashauri hivyo lazima madiwani wahakikishe wanasimamia kikamilifu ukusanyaji wa mapato.

Aidha alisema kuwa ili kuleta mafanikio lazima kila mmoja awajibike kwenye nafasi yake na kubwa ni katika kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Kibaha Musa Ndomba alieleza, watazingatia njia za ukusanyaji ili kufikia malengo yaliyowekwa ya ukusanyaji na watahakikisha fedha za miradi ya maendeleo zinatumika kutokana na thamani yà fedha (Value for Money).

Nae makamu mwenyekiti wa Halmashauri Selina Wilson alisema watahakikisha wanawaletea maendeleo wananchi,kusimamia ujenzi wa miundombinu na kufanya utatuzi wa migogoro mbalimbali ili wananchi waishi kwa amani. 

Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji Kibaha Jenifa Omolo alifafanua, Halmashauri itahakikisha inahudumia wananchi kwa kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kutumia mapato yanayokusanywa.

Madiwani walioapishwa ni 21 wote kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambapo 14 ni kutoka kwenye kata na watano ni wa viti maalum.

Awali kwenye uchaguzi wa mwenyekiti Musa Ndomba alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa Halmashauri kwa kupata kura 21 na makamu mwenyekiti Selina Wilson alipata kura 21.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...