Na Munir Shemweta, SIHA


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amesema sheria inaruhusu kuandikwa majina yote mawili ya wenza katika hati za umiliki ardhi.

Lukuvi alisema hayo tarehe 19 Desemba 2020 wilayani Siha mkoa wa Kilimanjaro alipokwenda kumaliza mgogoro wa ardhi baina ya Watawa wa Shirika la Kanisa Katoliki na wananchi wa kitongoji cha Mlangoni kuhusu Shamba la Kirari.

Alisema, Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imekuwa ikisajili Hati nyingi zenye majina yote mawili ya wenza na wengine husajili na majina ya watoto wao.

Kwa mujibu wa Lukuvi, siyo kweli kwamba Hati lazima isajiliwe kwa jina moja tu la mke au mume bali wote wawili wanaruhusiwa kitu cha msingi wawe na sifa za kumilikishwa.

Lukuvi alisema, hiyo ni fursa kwa wanawake kushawishi waume zao  katika kutekeleza suala hilo kwa kuwa sheria iko wazi  na hakuna Afisa Ardhi atakaye hoji suala hilo. 

"Akina mama mna ushawishi mkubwa  washawishini waume zenu waandike majina mawili ili kuepuka mgogoro" alisema Lukuvi

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliongeza kwa kusema kuwa, hata mtoto chini ya miaka 18 anaweza kusajiliwa katika hati kwa masharti kuandikwa pia jina la msimamizi.
 
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akiwasili katika kitongoji cha Mlangoni katika eneo la shamba la Kirari wilayani Siha mkoa wa Kilimanjaro kuhitimisha mgogoro wa ardhi uliodumu kwa miaka 40 baina ya Wananchi wa kitongoji hicho na Watawa wa Shirika la Kanisa Katoliki tarehe 19 Desemba 2020.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akisalimiana na mmoja wa Watawa wa Kanisa Katoliki katika ofisi ya halmashauri ya wilaya ya Siha mkoa wa Kilimanjaro wakati wa mazungumzo ya  kuhitimisha mgogoro wa ardhi katika Shamba la Kirari uliodumu kwa miaka 40 tarehe 19 Desemba 2020.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...