Vyuo Vikuu Nchini vimetakiwa kuzalisha wanafunzi wabunifu na wazalendo ambao wataweza kwenda kubuni miradi mbalimbali ambayo itawawezesha kujiajiri na kuajiri wengine ili kuweza  kutatua changamoto ya upatikanaji wa ajira nchini pindi wanapohitimu masomo yao ya elimu ya juu.

Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof. Kitila Mkumbo wakati akizungumza katika mkutano Mkuu wa Mwaka wa Majalisi Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Siku ya Alhamisi tarehe 17 Desemba 2020 ambao umeambatana na utoaji wa zawadi kwa wanafunzi wahitimu  211 ambao wamefanya vizuri katika masomo yao.

Prof. Mkumbo amesema kwa sasa nchi inahitaji vijana wabunifu na wazalendo ambao watakuwa chachu katika  kuwekeza katika miradi mbalimbali ikiwemo ya kilimo ,ufugaji, na uvuvi huku akiweka msisitizo kwa vyuo vikuu nchini kuwa na utaratibu wa kuwaandaa vijana katika kuwafundisha zaidi namna ya kujiajiri pasipo kusubiri ajira kutoka serikalini. “Lazima tubadilike kwenye ufundishaji wetu na tujue wanafunzi  wanasoma nini ,kwa sasa dunia imebadilika tunahitaji vijana wanaoweza kujiajiri kwa  hiyo sisi kama taasisi inayotoa elimu lazima tuwaandae vijana wetu zaidi kwenye kwenda kujiajiri, tukiweza kufanya hivyo na vijana wetu wakaelewa basi taifa letu litaondokana na changamoto  ya ukosefu wa ajira” alisema Prof. Kitila Mkumbo.

Kwa upande wake Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo upande wa Taaluma Prof. Maulid Mwatawala amesema SUA ni miongoni mwa vyuo ambavyo vinawaandaa wanafunzi zaidi kwenye kujiajiri na kusema kuwa SUA itakuwa mfano wa kuigwa nchini.“Mhe. Waziri nikuakikishie tuko vizuri, wanafunzi wote wanaosoma masuala ya kilimo, mifugo, uvuvi na masuala ya utalii hawa wote tunawaandaa ili waweze kujiajiri”alisema Prof. Maulid Mwatawala 

Katika mkutano Waziri wa Nchi,Ofisi ya Rais (Uwekezaji) Prof.Kitila Mkumbo  amemkabidhi mwanafunzi Musa Gese Doto tuzo mbili tuzo ya Mbunifu Bora wa Teknolojia ambapo amebuni gari shamba tuzo ambayo imetolewa na SETO TV na tuzo ya mbunifu bora wa Mwaka 2020 ambayo imetolewa na Tanzania Universities and Colleges Students Awards.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...