Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa, Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jeneral Marco Gaguti na timu ya Madereva wa Bodaboda kutoka mikoa hiyo miwili leo wamefanya ziara ya kutembelea na kujionea miradi mikubwa ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Magufuli kwenye Mkoa wa Dar es salaam.
 
Katika ziara hiyo wakuu hao wa mikoa na waendesha Bodaboda wamemtembelea Mradi wa Ujenzi wa reli ya kisasa SGR na jengo la abiria la Tanzanite, Mradi wa Mabasi ya mwendo wa haraka, Ujenzi wa stand mpya ya Mabasi ya Mbezi Luis, Daraja la Juu Ubungo na Mradi wa kufua umeme wa Kinyerezi two.
 
Akizungumza wakati wa ziara hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Mhe. Gelasius Byakanwa amesema wameamua kuwaleta waendesha Bodaboda kwenye ziara hiyo ili waweze kujionea Mambo mazuri na makubwa yanayofanywa na Serikali ya awamu ya tano ili wawe mabalozi wazuri kwa wenzao.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jeneral Marco Gaguti ameipongeza Serikali kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya Katika utekelezaji wa miradi yenye lengo la kutatua kero kwa wananchi.

Aidha Brigedia Jenerali Gaguti amesema mbali na ziara hiyo Jana pia walifanya mashindano ya Mpira wa moguu kati ya Timu ya Bodaboda Mtwara na Timu ya Bodaboda Kagera kwa lengo kujenga uzalendo kwa kundi hilo la vijana na kuwafanya kuwa mabalozi wazuri wa shughuli za Serikali.

 

 
*************************************

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...