Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa akisaini katika kitabu cha wageni katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera muda mchache baada ya kuwasili mkoa Kagera, huku akielekea jimboni Karagwe kwa ziara za mikutano katika kata mbalimbali ikiwa ni safari yake kwanza tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Wizara hiyo. Leo 30 Disemba 2020. (Picha na Eliud Rwechungura.)
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa (katikati) akiwa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Brigedia Jenerali Marco Gaguti (kushoto) na Katibu tawala wa Mkoa wa Kagera, Prof.Faustin Kamuzora (kulia) wakiteta jambo katika ofisi za Mkuu wa mkoa Kagera muda mchache baada ya kuwasili mkoani humo, huku akielekea jimboni Karagwe kwa ziara za mikutano katika kata mbalimbali ikiwa ni safari yake kwanza tangu alipoteuliwa kuwa Waziri wa Wizara hiyo. Leo 30 Disemba 2020.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...