Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo akielezea juu ya ziara ya wawekezaji na wafanyabiashara kutoka Uturuki katika studio za Radio Uhuru (Uhuru FM) Leo Jijini Dar es Salaam

Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo akiwa na wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Uturuki pamoja na wadau kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Chama cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA), Shirika la Viwanda Vidogo nchini (SIDO) na Mamlaka ya Kanda za Kusindika Usafirishaji Tanzania (EPZA) wakiwa tayari kwa kikao kazi. Wadau hao wamekutana kwa pamoja katika ofisi za TIC Jijini Dar es Salaam kuwaelezea wawekezaji kuhusu fursa mbalimbali za biashara zilizopo nchini. 


Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo (wa kwanza kushoto) pamoja na wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Uturuki wakifuatilia mada iliyokuwa inawasilishwa katika Ofisi za TIC, leo jijini Dar es Salaam


Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo (wa kwanza kushoto), wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Uturuki pamoja na wadau kutoka TIC, EPZA, TCCIA, TPSF na SIDO wakisikiliza mada iliyokuwa inahusu fursa mbalimbali za uwekezaji hapa nchini leo jijini Dar es Salaam


Balozi wa Tanzania nchini Uturuki, Mhe. Prof. Elizabeth Kiondo akiongea na wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya kumalizika kwa kikao baina ya Wawekezaji na Wafanyabiashara kutoka Uturuki pamoja na wadau kutoka TIC, EPZA, SIDO, TCCIA na TPSF Jijini Dar es Salaam 


Mwenyekiti wa Bodi wa Kampuni ya Kardag kutoka Uturuki ambae pia ni mmoja kati ya wawekezaji akiongea na wanahabari (hawapo pichani) mara baada ya kumalizika kwa kikao baina yao na wadau kutoka TIC, EPZA, SIDO, TCCIA na TPSF Jijini Dar es Salaam 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...