Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara Tanzania (MKURABITA) inaanza ziara ya ufuatiliaji wa utekelezaji wa shughuli za urasimishaji wa ardhi na biashara katika mikoa ya  nyanda za  juu kusini.

Akieleza kuhusu ziara hiyo Jijini Dodoma katika mahojiano maalum yaliyofanyika Januari 23, 2021, Mratibu wa Mpango huo, CPA, Dkt. Seraphia Mgembe amesema kuwa kamati hiyo itashiriki katika kazi mbalimbali ikiwemo zoezi la utoaji hati za hakimiliki za kimila za kumiliki ardhi katika halamshauri ya wilaya ya Mufindi mkoani Iringa na uwekaji wa jiwe la msingi la jengo la Ofisi ya masjala ya ardhi katika Kijiji cha Kapya wilayani Mbarali mkoani Mbeya.

Akieleza zaidi kuhusu ziara hiyo Dkt. Mgembe amesema kuwa ziara hiyo ya wiki moja inaanza leo Januari 24, 2021  hadi Januari 31,2021.

MKURABITA imekuwa ikiwezesha wanachi kipitia urasimishaji ardhi na biashara katika halmashuri mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kuwawezesha kiuchumi kama ilivyo dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano.

Mratibu wa Mpango huo, CPA, Dkt. Seraphia Mgembe


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...