Mwanamitindo Naomi Campbell amekubali uteuzi wa kuwa balozi wa kimataifa wa Utalii Kenya.

Kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya Utalii na Wanyamapori, makubaliano hayo yamefikiwa kati ya Campbell na waziri wa utalii na wanyamapori, Najib Balala.

“Tunafurahishwa na taarifa kuwa Naomi Campbell atakuwa balozi wa utalii na kusafiri kimataifa akitangaza Kenya” Waziri amesema.

Wakati wa mkutano huo, Naomi Campbell alisifu serikali ya Kenya kwa kuimarisha miundombinu katika eneo la pwani ikiwa ni pamoja na kuimarisha uwanja wa ndege wa Malindi kuwa wa hadhi ya kimataifa na kuongeza kuwa hatua hiyo itaimarisha utalii katika eneo hilo.

Mwanamitindo huyo maarufu duniani atasaidia kuitangaza Kenya kama eneo ambalo ni kivutio cha utalii duniani.

Bi Campbell amekuwa  akitembelea mara kwa mara eneo la Malindi kuvinjari nyakati za mapumziko yake.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...