Wanaakiolojia wamegundua zana za mawe zilizotumika miaka milioni mbili iliyopita na binadamu wa kale zaidi katika eneo la Bonde la Olduvai, Kaskazini mwa Tanzania.
Ugunduzi huo unatoa mwanga mpya juu ya namna binadamu wanaoaminika kuwa ni wa kale zaidi walivyoishi na kuyamudu mazingira yao. Ugunduzi huo pia unatoa jibu la kwamba, binadamu wa kale aliishi miaka milioni mbili iliyopita na sio milioni 1.8 kama ilivyogundulika na watafiti wa awali.
Ugunduzi huo ni matokeo ya utafiti uliochukua miaka mitatu na ulihusisha watafiti kutoka ndani na nje ya Tanzania.
''Tulianza utafiti mwaka 2017, ikatuvutia tukarudi mwaka 2018, tukitoka Olduvai tunarudi maabara, maabara tunakutana na changamoto, tukaendelea kutafiti, kwa sababu tulitaka tufanye kisayansi kabisa, tuliendelea hivyo ili tusiache mashaka hata kidogo kuhusu miaka laki mbili iliyoongezeka,'' alisema Dkt. Pastory Bushozi, Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, ambaye alikuwa mmoja wa watafiti washiriki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...