Milolongo mirefu imeshuhudiwa katika vituo vya kupigia kura katika mji mkuu Kampala, na maeneo menginge ya nchi

Serikali imeamuru kufungwa kwa mitandao yote ya kijamii.

Shughuli ya kupiga kura ilipangwa kuanza saa moja asubuhi na kukamilika saa kumi jioni kwa saa za Uganda, ingawa Tume ya uchaguzi nchini humo ilisema kuwa wapigakura wote waliojisajiri ambao watakuwa bado katika mstari wa kupiga kura wakati shughuli hiyo itakapofungwa, wataruhusiwa kupiga kura yao.

Mgombea wa urais wa upinzani Bobi Wine anatarajiwa kupiga kura yake katika kituo kilichopo viungani mwa mji mkuu Kampala.

Rais Yoweri Museveni atapiga kura yake kijijini kwao magharibi mwa Uganda.

Baadhi ya wanadiploamsia wameelezea wasi wasi wao juu ya mchakato wa uchaguzi, wakielezea kukamatwa kwa wapinzani wakati wa kampeni zilizogubikwa na gasia.

Pia wamezungumzia dhidi ya mashambulio dhidi ya uhuru wa kujieleza, baada ya serikali kuwaambia watoaji wa huduma za intaneti kukata huduma zao.

 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>>>

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...