*Zeeland aahidi kuwachukulia hatua Watendaji hao
Na Chalila Kibuda,Michuzi TV
MBUNGE wa Mvomero Jonas Zeeland amesema wapo baadhi ya watendaji wanafanya uzembe wakutopeleka fedha za mfuko wa Jimbo kwenye miradi.
Akizungumza katika wa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Mvomero , Zeeland amesema fedha za miradi mpaka Sasa bado hazijafika na tayari zimeshazigawanywa kwa kata zote na kuahidi kuanzia sasa mtendaji yeyote atayezembea au kuzitumia fedha hizo kinyume na utaratibu atachukuliwa hatua za kinidhamu.
"Ninaomba fedha ambazo tumezigawanya ziende sasa na mimi Mbunge wenu nataka twende kwa Kasi kubwa kutekeleza miradi na kutatua changamoto za wananchi ikiwemo ukusanyaji wa mapato nao tuongeze nguvu"amesema Zeeland
Mbunge Zeeland amesema ameshafanya mawasiliano na Waziri wa Maliasili na Utalii amekubali kufanya kikao na uongozi wa Halmashauri ya Mvomero kwa ajili ya kutatua kero ya wanyama wakali tembo ambao wanapoteza maisha ya wananchi.
Amesema kikao hicho kitafanyika Februari wakati wowote tujiandae katika kutatua tatizo mara moja.
"Mimi ni mbunge wenu wa Jimbo hili la Mvomero kwa kushirikiana na Mwenyekiti wa Halmashauri na Mkurugenzi tumeanza sasa kuzifanyia kazi changamoto mbalimbali kutokana na ziara ambazo nimefanya maeneo mbalimbali ya Jimbo." amesema Zeeland.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...