Na Zainab Nyamka, Michuzi Tv
Mkuu
wa Wilaya Kigamboni Sara Msafiri amewataka wananchi wa Kigamboni
kutumia huduma ya maji kutoka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira
Dar es Salaam (DAWASA) na kuachana na maji ya visima.
Aidha,
amesema mamlaka pekee iliyopewa dhamana ya kutoa huduma ya maji ni
Dawasa, kama mwananchi una kisima chako hautaruhusiwa kutoa huduma ya
maji kwa watu wengine
Hayo ameyasema wakati mkutano na wananchi wa Kigamboni akisikiliza kero mbalimbali zinazowakabili ili ziweze kutatuliwa.
Amesema,
kumekuwa na kero mbalimbali ambazo aliweza kuzipokea kutoka kwa
wananchi kuhusiana na huduma ya maji ya maji inayotolewa na Dawasa na
leo wamefika wote kwa pamoja ili kuhakilisha zinaisha
Mapema
wiki iliyokwisha kulikua na Kliniki ya kusikiliza kero za wananchi
ndani ya Wilaya ya Kigamboni, kupitia taasisi mbalimbali za kiserikali
na kugundua Dawasa inabidi iongeze siku tatu za ziada za kusikiliza kero
hizo karibu na maeneo wanayotolea huduma
"Niliwaambia
Dawasa waje maeneo haya wasikilize kero za wananchi lakini nimeambiwa
hapa ndani ya siku tatu ni wananchi 25 tu ndo wamefika na kusikilizwa na
sisi kama serikali tutayafanyia kazi hayo malalamiko," amesema Sara.
Ameeleza,
wananchi wamekuwa na malalamiko mengi wanaongelea pembeni lakini
wanapoletewa wahusika ili waelezee kero zao wamekuwa hawafiki jambo
ambalo linaamisha kuwa kila kitu kipo sawa na kuishia kuongea pembeni.
"Nimesikia
kero ya Bili ya maji na maunganusho mapya, ukiachilia mbali mnataka
huduma ya maji Visima kurudishwa niweke wazi Dawasa ndio mamlaka
iliyopewa dhamana ya kutoa huduma ya maji kwa Dar es Salaam na miji ya
Pwani, kwa bei elekezi kutoka Ewura," amesema.
"Hivyo
msitarajie huduma hiyo kurudi, na hata hao wamiliki wakati wanapewa
leseni ili wachimbe visima waliambiwa mtandao wa Dawasa utakapofika basi
watasitishiwa huduma hiyo,"
Naye
Kaimu Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki Mhandisi Amani Nyekela amesema
DAWASA ni moja ya Mamlaka inayofanya nao kazi kwa ukaribu sana.
Akielezea bei ya maji inayotolewa na Dawasa ni elekezi na inatumika kwa maeneo yote ikipitishwa na Ewura.
Akizungumzia
miradi ya maji Kigamboni, Meneja Kihuduma Kigamboni Tumaini Muhondwa
amesema uendelezaji wa visima hivyo katika mradi wa visima vya Kimbiji
utagharimu Bilioni 10.5 kwa fedha za ndani kujenga miundo mbinu na
unatarajia kukamilika ndani ya miezi 15.
Amesema,
Uendelezaji wa visima umegawanyika katika hatua za ujenzi wa tanki la
kuhifadhia maji, ujenzi na ulazaji wa bomba la kusafirisha majj km 5.7,
ujenzi wa kituo cha kupokea maji kutoka kwenye kisimana na ufungaji wa
pampu za umeme kwa ajili ya kuendesha mitambo.
Muhondwa
ameeleza, kazi ya usanifu imeanza kupitia mshauri WAPCOS na tanki la
maji litajengwa eneo la Kichangani kupitia Kisima cha Kifurukwe na
ulazaji wa bomba la usambazaji Km 23.9 na utahudumia maeneo ya
Kifuruku, Kiziza, Uvumba na Kichangani.
"Sehemu
ya pili ujenzi wa bomba kwa umbali wa Km 27 litakalounganishwa na bomba
lililovushwa darajani kutoka Ruvu Chini mradi huu utahudumia maeneo ya
Kigamboni, Ferry, Tungi, Magogoni na Upendo,"
Mbali
na hilo, Dawasa wamewataka wananchi kuendelea kujitokeza kwa wingi
katika ofisi zao kwa ajili ya kupatiwa huduma ya maji na kwa sasa wana
zaidi ya wateja 3400 wanaopata huduma ya maji safi na salama.Mkuu wa Wilaya Kigamboni Sara Msafiri akizungumza na
wananchi waliojitokeza kwa ajili ya kusikiliza na kutatua changamoto ya
Maji ndani ya Mkoa wa Kihuduma Dawasa Kigamboni. wa pili Kulia ni
Meneja wa Wa Dawasa Mkoa wa Kihuduma Kigamboni Tumaini Muhondwa. Mkutano
huo umefanyika katika Viwanja vya Swala Wilaya ya Kigamboni.
Meneja wa DAWASA Mkoa wa Kihuduma Kigamboni Tumaini Muhondwa akitoa
taarifa ya mradi wa maji wa Kimbiji unaoendelea kutekelezwa na Mamlaka
hiyo kwa kutumia fedha za ndani utakaoondoa kero ya maji kwa Mji wa
Kigamboni na maeneo ya karibu.
Mkuu
wa Wilaya Kigamboni Sara Msafiri akimsikiliza moja ya wananchi
waliofika katika Viwanja vya Swala Kigamboni kutoa kero na changamoto
mbalimbali.Kaimu Meneja wa EWURA Kanda ya Mashariki Mhandisi Amani
Nyekela amesisitiza wananchi kutumia nafasi zao kutoa maoni kupitia njia
rasmi ya kupiga simu kwa Mamlaka hiyo ili kuweza kutatua changamoto
zinazojitokeza katika sekta ya maji, umeme, gesi na mafuta. EWURA
wameshirikiana na DAWASA kuweza kusikiliza na kutoa elimu juu ya huduma
ya maji inayotolewa na Mamlaka ya Maji Dawasa Ndani ya Jiji la Dar es
Salaam na Miji ya Pwani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...