NA  YEREMIAS  NGERANGERA…NAMTUMBO

Mkurugenzi  mtendaji wa  Halmasjhauri ya wilaya  Namtumbo  mkoani Ruvuma  Evance  Nachimbinya  amewaagiza  watendaji wa vijiji  na kata katika Halmashauri hiyo  kukusanya mapato  kupitia vitambulisho vya ujasiliamali ,kukusanya mapato  yatokanayo  na kodi ya  majengo  pamoja na mabango.

Akiongea  na watendaji wa  kata na vijiji  katika ukumbi wa Halmashauri hiyo Nachimbinya alisema  kodi ya  majengo na mabango  ilikuwa inakusanywa na mamlaka ya Mapato  Tanzania TRA lakini  kwa sasa serikali imerudisha serikali za mitaa ili kurahisisha ukusanyaji huo .

Hata  hivyo bwana  Nachimbinya  aliwaagiza watendaji hao  kuwa kabla ya kuanza ukusanyaji huo  watendaji wanatakiwa kuwasilisha  taarifa za majengo yanayostahili kulipiwa kodi  pamoja na idadi ya mabango yanayotakiwa kulipiwa  yaliyopo katika vijiji vyao katika ofisi ya mkurugenzi .

Awali  afisa biashara  wa Halmashauri ya wilaya ya Namtumbo  bwana  Revocatus  Kavishe  aliwaambia watendaji hao kuwa  wanatakiwa  kufuata sheria taratibu na kanuni  katika  kusajiri  walipa kodi za  majengo na  sio kupokea maelezo ambayo yanayolenga  kukwepa  kulipa kodi na   kimsingi hayapo  katika sheria.

Kavishe  alidai  uzoefu  unaonyesha  kuwa wapo watendaji  katika kutekeleza majukumu yao  huwa  hawasimamiii  kanuni na sheria zilizopo na badala yake  husikiliza maelezo  ya watu  wenye nia ya kukwepa  ambayo  hayapo  katika  kanuni  na sheria zilizopo .

Alitaja  uzoefu  alioupata katika  ukusanyaji wa  fedha za vitambulisho  vya ujasiliamali alidai wapo watendaji ambao hawakuuza vitambulisho  kwa baadhi ya wafanyabishara wadogo  kutokana na  kusikiliza maelezo  na kuacha kuwauzia vitambulisho badala ya kufuata sheria  na kanuni zilizopo za wanyasiliamali wote wanahitajika kuwa na vitambulisho badala ya kupokea maelezo.

Mario  Mwageni  mtendaji  wa mamlaka  ya mji  mdogo wa  Namtumbo kwake yeye  zoezi hilo  alidai sio geni lakini alihoji sheria ya ukusanyaji inasemaje katika maeneo mengine ambayo sio mamlaka ya miji midogo  kwa kuwa  ukusanyaji katika sheria  inayotumika inaishia kukusanya  kodi ya majengo  mwisho katika mamlaka  ya miji midogo pekee.

Afisa  kodi ya majengo kutoka  mamlaka ya mapato  wilaya ya Namtumbo  bwana  Samwel  Masawe aliyehudhuria kikao hicho  alidai nyumba zinzotakiwa kulipiwa kodi ya jengo ni zile zilizojengwa kwa tofali na kuezekwa  bati  huku  ndani ya nyumba hizo  kuna watu wanaishi. Alifafanua bwana Masawe.

Afisa  utumishi  wa Halmashauri hiyo  Eleonora  Lyimo  pia alitumia nafasi hiyo kuwataka watumishi  kuitisha vikao  kwa mujibu wa sheria  huku akiwasihi  kufanya kazi zinazowapasa kufanya  na kuacha kujiingiza katika makundi ya siasa  pamoja na kujikita katika  swala la ulevi  kupindukia na kusahau  kazi.



 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...