Na Linda Shebby, Pwani

Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani  linamshikilia  mtuhumiwa   mmoja mwanaume Shaaban Rashid Athumani   mwenye umri wa miaka 61 mkazi lwa Kwamakocho , Kata ya Mamdela  Wilayani Chalinze Mkoa wa Pwani kwa kosa la kumili  Kiwanda cha kutengeneza silaha  za kienyeji(gobole).

Yamesemwa hayo na Kamanda wa Jeshi la Polisi  Mkoa wa Pwani (RPC), Nyigesa Wankyo kwamba mnamo Januari 31 mwaka 2021 majira ya saa moja usiku katika  eneo tajwa hapo juu , Jeshi  la Polisi lulimkamata  akiwa na vifaa  vya kutenfengezea  silala aina ya gobole na vingine ikiwa ni pamoja na  Mtambo  wa kufulia vyuma,chupa tano na  ndogo zenye baruti ndani   yake,faraki 48,risasi 42 za bunduki  aina ya gobole, paketi  moja ya unga wa  kiberiti,mitambo  mitatu  ya silaha  aina ya gobole, ambayo  ipo tayari bado kuwekwa kwenye silaha  aina ya gobole na kopo moja  lenye tindikali  ambao una tumika  kuunganisha  vyuma  vinavyifungwa kwenye  silaha  aina ya gobole.

RPC Wankyo amesemamkuwa pia jeshi hilo 
limekamata  limekamata silaha na risasi zake" mnamo Januari 21  mwaka huu  majira ya saa 6:30usiku katika maeneo ya Pingi Wilaya ya Kipolisi  Chalinze Mkoa wa  Pwani  walifanikiwa  kumkamata  mtuhumiwa  mmoja jina limeifadhiwa  kwa kosa la kumiliki bunduki tatu  Shortgun mbili na gobole moja , risasi 13 za shortgun, maganda matatu  ya risasi, coocking handle mbili, goroli 60,misumeno miwili ya kukatia  mbao  na chuma, pia alikamatwa na Plaizi moja , bisibisi moja, kipande cha mtutu wa bunduki, vipande vidogo vya vyuma  sita, vipande vya miti vyenye  chuma  ndani vinne, mitambo ya kutengenezea  bunduki viwili, juhudi za kuwatafuta watuhumiwa wengine katika tukio hili zinaendelea alisema RPC  Wankyo.
Aidha RPC  Wankyo aluongeza kwa kusema kuwa  Jeshi la  Polisi  Mkoa wa Pwani  linawashikilia  watuhumiwa  wawili wote wanaume  amvao ni Mtuli  Mhode Chapalisi mwenye umri wa miaka (52) kabila Mmasai na Reuben Krekereni Oyela  mwenye umri wa miaka( 31) kabila Masai ,mtuhumiwa mwingine ni  Hamisi RongwinyoChambuli mwenye umri wa miaka( 67) wote hawa ni wafugaji  kwa kosa la kung'oa  na kuharibu  mazao  (miche ya mikorosho)  kwenye shamba lenye ukubwa hekari saba  mali ya Reuben Mkandala na John Simon Biginagwa (marehemu kwa sasa) aliyekua  mtumishi  katika ofisi  ta Mkuu wa Mkoa wa Pwani.

Kwa pamoja  watuhumiwa  hao   na wenzao  ambao bado   wanatafutwa waling'oa miche   hiyo katika shamba  tajwa Januari 27 mwaka huu saa nane mchana  katika kitongoji cha Ribaya , Kijini cha Diozile Wilaya ya Kipolisi Chalinze Mkoa wa Pwani na kusababisha hasara ya 50,000,000.
Wakati huohuo RPC Wankyo amesema kuwa  kumerokea ajali  ambapo gari imeacha njia nan kupinduka  na kusababisha uharibifu wa gari.

"Ajali hiyo  imetokea jana Januari mosi mwaka huu majira ya saa mbili usiku  huko Mdaula  Wilayani Chalinzr   Mkoa wa Pwani ambapo  gari lenye namva  T.991DFH Howo lenye  trela T. 801CLM  lililokuwa  limebeba  mafuta aina ya  dizeli likiendeshwa na dereva Masoud Abdallah  mwenye umri wa miaka (46) kavila Mnyiramva Mkaazi wa Kimara Jijini  Dar es Salaam.

"Alipata ajali hiyo  akitokea  Dar es Salaam kwenda Zambia   baadanya kuacha  njia na kupinduka   na kusababisha uharibifu wa  gari  hilo, chanzo cha ajali  ni dereva kuendesha  gari huku akiwa amelewa pombe,baada ya kupekuliwa  kwenye gari alikutwa  na pombe aina ya K- Vant iliyokua  imetumika  na chupa , Jeshi la Polisi linatoa rai kwa wananchi kuacha  uhalifu na kuacha kuendesha  vyombo  vya moto   huku wakiwa wamelewa"

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...