Diwani wa Kata ya Kivule Nyasika Getama akizungumza  January 30/2021katika kikao cha Serikali ya Mtaa Kivule ambapo alialikwa kuwa mgeni rasmi, katika hotuba yake Diwani Nyasika alielezea kukuza sekta ya Elimu na kuwaimiza WANANCHI kukata Bima ya Afya iliyoboreshwa kwa ajili matibabu.
Afisa Maendeleo Kata ya Kivule Anna Masawe akizungumza Jana January 30/2021 katika kikao cha Serikali ya Mtaa Kivule akiwataka Wanawake,Vijana na Watu wenye ulemavu kuunda vikundi Wasajili waweze kupata mikopo ya Serikali
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Kivule Amos Hangaya akizungumza katika kikao chake cha WANANCHI kinachojadili Maendeleo pamoja na kupokea kero January 30/2021 (kulia) Diwani wa Kata hiyo Nyasika Getama na Afisa Mtendaji wa Mtaa.

Na Heri Shaaban
SERIKALI ya Mtaa Kivule inatarajia kufungua soko la Kivule February Mwaka huu kwa Wafanyabiashara wote wa kata hiyo. 

Akizungumza katika mkutano wa adhara ulioandaliwa na Serikali ya Mtaa Kivule Halmashauri ya Ilala Dar es salaam jana ,Mwenyekiti wa Mtaa Kivule Amos Hangaya alisema alhamisi Febuary 4 Mwaka huu wanawaita Wafanyabiashara wote kwa ajili ya kuwatambua upya pamoja na kugawa vizimba vya Biashara amewataka wafanyabiashara wote kujitokeza siku hiyo. 

Mwenyekiti Amos alisema kwa sasa soko hilo litatumika kwa dhumuni lililolusudiwa soko sio Mnada,Gulio watawatafutia utaratibu kwa ajili ya kuendesha minada yao  kila wiki. 

"Nawaomba Wafanyabiashara wote ambao walipewa vizimba katika soko hili kujitokeza siku hiyo kwa ajili ya kuwatambua rasmi soko linataka kufunguliwa hivyo wote mnatakiwa kufanya biashara sehemu rasmi ambazo zimetengwa na sio mitaani au barabarani " alisema Amos. 

Amos alisema Serikali  ya awamu ya tano TANZANIA ya Uchumi wa viwanda inayoongozwa na Rais John Magufuli inataka wananchi wake wafanye biashara ili wajikwamue kiuchumi sambamba na kuunda viwanda vidogovidogo  ili wapate kipato.

Aliwataka wakazi wa Kivule kuunga mkono juhudi za Rais John Magufuli katika kufanyaji kazi na kuleta maendeleo pamoja na kusimamia miradi ya Serikali ambayo ipo katika eneo hilo.

Wakati huo huo Mwenyekiti Amos alisema moja ya Mikakati yake mingine kuanzisha ruti mpya ya Daladala Kivule Sokoni kwenda Mnazi  Mmoja inatarajia kuanza Wiki hii nauli bei yake shilingi 400/= na ukipanda ufikishwe mwisho wa gari usikubali kushushwa njiani kwa ili wakatishe ruti.

Amos alisema utaratibu wa ruti hiyo daladala hizo umeshakamilika kila abiria akipanda adai tiketi jambo lolote likitokea  atoe taarifa 
Mamlaka husika.

Kwa upande wake Mgeni rasmi Diwani wa Kata ya Kivule Nyasika Getama aliunga mkono juhudi hizo hatawasaidia ili malengo yaweze kutimia 

 Diwani Nyasika aliwataka WANANCHI wa Kata hiyo kukata bima ya afya kwa ajili  matibabu kwani maisha  ya mwanadamu matibabu gharama kubwa hivyo kuna umuhimu wananchi wa kata ya kivule wote wawe na Bima ya afya

Alisema kwa sasa Serikali imerahishisha imetoa Bima iliyoboreshwa kwa ajili ya wananchi wote  kuanzia ngazi ya familia hadi mtu mmoja. 

Akielezea sekta ya elimu alisema kata ya Kivule ipo Ilala Vijijini matokeo ya mwaka  huu shule ya sekondari wamepata alama A ufaulu mzuri na maadili kitaaluma yapo vizuri amewataka wazazi kufatilia maendeleo ya watoto wao na kushirikiana na Walimu wa Msingi na Sekondari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...