Gomes ameweka wazi kuwa anatambua mchezo huo ni mgumu sana ukizingatia uzoefu wa wachezaji wengi wa As Vita sambamba na mbinu za Kocha Mkuu wa AS Vita, Florent Ibenge.
Amesema, anaamini wachezaji wake watapambana ili kupata matokeo chanya na kujinyakulia pointi tatu muhimu.
Aidha,
Simba katika msimu wa mwaka juzi wakiwa wanashiriki michuano hiyo ya
kimataifa, waliweza kupoteza mchezo wao dhidi ya As Vita kwa mabao 5-0.
Hiki ni kikosi ambacho kinatarajiwa kuanza leo mbele ya AS Vita ugenini:-
Aishi Manula
Shomary Kapombe
Joash Onyango
Ame Ally
Erasto Nyoni
Thadeo Lwanga
Mzamiru Yassin
Junior Lukosa
Luis Miquissone
Clatous Chama
Benard Morrison
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...