Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu hii leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Chakula Duniani (WFP) Bi. Sarah Gordon – Gibson katika Ofisi ndogo ya Makamu wa Rais Jijini Dar es Salaam. Katika mazungumzo yao wamekubaliana kushirikiana katika jitihada za  kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi na uharibifu mazingira nchini kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa chakula.

Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Chakula Duniani Bi. Sarah Gordon – Gibson akifafanua jambo kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu katika Ofisi ndogo ya Makamu wa Rais Jijini Dar es Salaam. 

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu na Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Chakula Duniani Bi. Sarah Gordon – Gibson wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kikao baina yao kilichofanyika hii leo, jijini Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...