Wafanyakazi wa Benki ya Equity Tanzania wameungana na wateja wao katika maadhimisho ya ‘Siku ya Wanawake Dunia 2021’. Katika halfa hizo zilizofanyika katika matawi yote ya Benki hiyo nchini, wateja walipata warsa wa kukutana na wafanyakazi na viongozi wa Benki hiyo na kufurahi kwa Pamoja.
Siku
ya Wanawake duniani ambayo husherehekewa kila tarehe 8 Machi, ina lengo
la kukutanisha wadau mbalimbali ili kutambua mchango wa wanawake na
kutatua changamoto zinazowakabili.
to challenge” au “amua kupambana” ikihamasisha uwepo wa usawa wa kijinsia katika jamii na mahali pa kazi.
Akizungumza
katika hafla iliyofanyika katika tawi la Mwenge jijini Dar es Salaam,
Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya Equity Tanzania, Esther Kitoka
alisema Benki ya Equity inachukulia kwa umuhimu suala la kumuwezesha
mwanamke na ndio maana imeweka bidhaa mahususi na huduma za mikopo nafuu
kwa ajili ya kinamama.
“Equity
Bank tunatoa bidhaa maalum kwa wanawake kama Eazzy-Kikundi na mikopo
nafuu ya Fanikisha tukilenga kuleta mapinduzi ya kiuchumi kwa mwanamke
mmoja mmoja kama mjasiliamari au wale walioko kwenye vikundi kama
Viccoba na vinginevyo. Nichukue fursa hii kuwakaribisha akina mama wote
Equity Bank” alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...