Wafanyakazi wa Benki ya Equity Tanzania wameungana na wateja wao katika maadhimisho ya ‘Siku ya Wanawake Dunia 2021’. Katika halfa hizo zilizofanyika katika matawi yote ya Benki hiyo nchini, wateja walipata warsa wa kukutana na wafanyakazi na viongozi wa Benki hiyo na kufurahi kwa Pamoja. 

Siku ya Wanawake duniani ambayo husherehekewa kila tarehe 8 Machi, ina lengo la kukutanisha wadau mbalimbali ili kutambua mchango wa wanawake na kutatua changamoto zinazowakabili.


to challenge” au “amua kupambana” ikihamasisha uwepo wa usawa wa kijinsia katika jamii na mahali pa kazi.

Akizungumza katika hafla iliyofanyika katika tawi la Mwenge jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mwendeshaji wa Benki ya Equity Tanzania, Esther Kitoka alisema Benki ya Equity inachukulia kwa umuhimu suala la kumuwezesha mwanamke na ndio maana imeweka bidhaa mahususi na huduma za mikopo nafuu kwa ajili ya kinamama.
 

“Equity Bank tunatoa bidhaa maalum kwa wanawake kama Eazzy-Kikundi na mikopo nafuu ya Fanikisha tukilenga kuleta mapinduzi ya kiuchumi kwa mwanamke mmoja mmoja kama mjasiliamari au wale walioko kwenye vikundi kama Viccoba na vinginevyo. Nichukue fursa hii kuwakaribisha akina mama wote Equity Bank” alisema.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...