LIGI kuu ya Vodacom Tanzania bara imeendelea tena leo mechi ya  mapema imewakutanisha  wenyeji wa mchezo huo KMC FC ambao walikuwa wakiwakaribisha  Ruvu Shooting kutoka huko mkoani Pwani.

Mechi hiyo imemalizika kwa KMC FC kuondoka na alama tatu muhimu kwa kuwafunga Ruvu Shooting goli moja kwa bila,Goli pekee la KMC limefungwa na beki wao Lusajo Mwakenda kunako dakika 35 ya mchezo.

Matokeo haya yanaifanya KMC FC kutoka nafasi ya saba mpaka nafasi ya tano  ambayo ilikuwa ikishikiliwa na Ruvu Shooting.

KMC FC sasa wanafikisha alama 35 huku Ruvu Shooting wakibakiwa na alama zao  34  wakishika nafasi ya sita kwenye msimamo wa ligi kuu Tanzania bara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...