RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akifuatilia muktasari wa
taarifa ya utekelezaji wa maagizo yake aliyoyatoa kwa Mawaziri na
Makatibu Wakuu wakati wa kuwaapisha, ikiwasilishwa na Waziri wa Ujenzi
Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Mhe. Rahma Kassim Ali, mkutano huo
umefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
KATIBU Mkuu Wizara ya Ujenzi
Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Ndg.Amour Hamil Bakar, akiwasilisha
taarifa ya utekelezaji wa maagizo ya Rais alilyoyatoka kwa Mawaziri na
Makatibu Wakuu wakati wa kuwaapisha katika viwanja vya Ikulu, mkutano
huo umefanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar na (kushoto)
Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi Mhandisi Zena
Ahmed Said.(Picha na Ikulu)
WAKUU wa Idara na Taasisi za
Wizara ya Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, wakifuatilia taarifa
ya utekelezaji wa Maagizo ya Rais aliyoyatoa wakati wa kuwaapisha kwa
Mawaziri na Makatibu Wakuu, ikiwasilishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya
Ujenzi Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar Ndg.Amour Hamil Bakar, wakati wa
mkutano huo uliofanyika katika ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar.(Picha
na Ikulu)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...