Na Mwandishi wetu, Chato

WACHIMBAJI madini nchini wote kwa umoja wao kesho Ijumaa Machi 26 wakati jeneza lenye mwili wa Rais wa awamu ya tano Hayati Dkt John Joseph Pombe Magufuli utakaposhushwa rasmi kaburini wanapaswa kusimama walipo kwa muda wa dakika tano.

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Wachimbaji Madini Tanzania (FEMATA) Lister Festo Balegele amesema wachimbaji wote wa madini nchini wanapaswa kufanya hivyo ili kutoa heshima zao za mwisho popote walipo.

"Tunapaswa kufanya hivyo kutokana na msiba mkubwa uliolikumba Taifa la kuondolewa na kipenzi chetu wachimbaji wadogo kwani alitupigania kwa nguvu zake zote," amesema Balegele.

Amesema ule muda utakaotangazwa wa kushusha rasmi jeneza la marehemu hayati Dokta Magufuli kwenda kaburini inatakiwa wachimbaji wote wasimame walipo kwa muda wa dakika tano ili kumuenzi.

"Kila mmoja atakapokuwa hata kama upo mgodini tunaomba usimame pembeni kwa dakika tano tuu ili kutoa heshima za mwisho kisha uendeleee na shughuli yako," amesema Balegele.
 Rais wa FEMATA John Bina (kushoto) na Katibu wa FEMATA Lister Festo Balegele wakiwa Wilayani Chato Mkoani Geita, kwenye msiba wa Rais wa awamu ya tano hayati Dkt John Magufuli.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...