Na Mwandishi wetu, Babati
ZAIDI
ya wananchi 239,858 Mkoani Manyara, wanatarajiwa kunufaika na huduma ya
maji kwenye vijiji 87 ambapo kumetengwa vituo vya umma 617 vya kuchotea
maji.
Meneja
wa wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (Ruwasa) Mkoani
Manyara, mhandisi Wolta Kirita ameyasema hayo mjini Babati kwenye siku
ya wadau wa maji.
Mhandisi
Kirita amesema wananchi hao wa vijiji hivyo 87 watakaonufaika na huduma
hizo za maji ni kutoka wilaya za Simanjiro, Kiteto, Mbulu Hanang' na
Babati.
Amesema Ruwasa
mkoani Manyara, kwa mwaka wa fedha wa 2021 wamepanga kukusanya na
kutumia sh18 bilioni kwa ajili ya kujenga, kukarabati na kuongeza
mitandao ya maji.
Amesema
miongoni mwa vipaumbele vyao kwa mwaka 2021/2022 ni ujenzi wa miradi
mipya ili akiba ya kutosha iliyo tayari kutekelezwa wakati wowote pindi
fedha zikipatikana.
"Pia
vipaumbele vingine ni kupeleka huduma ya maji katika vituo vya afya,
zahanati, shule za msingi na sekondari ambazo hazina huduma ya maji,"
amesema mhandisi Kirita.
Mkuu
wa mkoa wa Manyara, Joseph Mkirikiti amewapongeza Ruwasa kwa namna
wanavyotekeleza miradi mbalimbali ya maji kwa wananchi waliopo kwenye
wilaya za eneo hilo.
Mkirikiti
amesema hata hivyo wananchi wa mkoa huo wanapaswa kujenga miundombinu
ya kuvuna maji kwenye maeneo wanayoishi na taasisi za Serikali pindi
mvua zinaponyesha.
"Kuliko
kulalamikia ukosefu wa maji ni bora kuyavuna pindi mvua zinaponyesha,
kwa wale mliofika wilaya ya Newala Mkoani Mtwara mtaona kila nyumba ina
miundombinu ya kuvuna maji tuige hayo mambo mazuri," amesema Mkirikiti
Naibu
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul amesema bado wananchi wa mji
wa Babati wanalalamikia bei kubwa ya maji kupitia ankara tofauti na miji
mingine nchini.
Gekul
amesema amekuwa akilielezea hilo kila wakati na hata Bawasa
wanapopunguza kwa sh40 wananchi wanaona bado wanatozwa bei ghali tofauti
na maeneo mengine nchini.
Meneja wa wakala wa maji na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) Mkoani
Manyara, mhandisi Wolta Kirita akizungumza Mjini Babati, kwenye siku ya
wadau wa maji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...