Na Richard Mwamakafu - WHUSM, Dar es Salaam

Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa ametoa pongezi kwa Tume ya Ushindani nchini (FCC) na Timu ya Soka ya  Simba SC   kwa kumaliza mgogoro wao na kusisitiza vilabu vingine vya soka kuiga mfano huo ili kuleta  maendeleo ya mchezo wa soka nchini.

Mhe.Bashungwa ametoa pongezi hizo leo Aprili 24, 2021 alipotembelea   Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha michezo cha Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF) kilichopo  Kigamboni, Dar es Salaam

"Navikaribisha Vilabu vingine kushirikiana na  Serikali  ili kuendana na Dira ya Serikali na maelekezo ya Rais wetu Mhe. Samia Suluhu Hassan ya kutaka Sekta hii kutoa ajira kubwa sana kwa vijana na kuchangia kwenye pato la nchi"

Mhe.Bashungwa ametumia nafasi hiyo pia kuipongeza timu ya Simba kwa kufika hatua ya robo fainali katika Michuano ya Klabu Bingwa Afrika, huku akiwasihi Watanzania    kuonyesha  uzalendo wa kuiunga mkono timu hiyo   inayoitangaza nchi ya Tanzania kimataifa na kupitia  kauli mbiu ya timu hiyo ya (Visit Tanzania) "Tembelea Tanzania" katika Jezi zao.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...