Na Said Mwishehe, Michuzi TV
BARAZA
Kuu la Waislamu Tanzania(BAKWATA)limetoa tamko kulaani vitendo vya
kinyama na uadui dhidi ya Taifa la Palestina na kuuwa rais wasio na
hatia.
Akizungumza leo Mei 20,2021 jijini Dar es Salaam, Sheikh
Mkuu na Muft wa Tanzania Abubakar Zubeir amesema Baraza Kuu la Waislamu
Tanzania linalaani vitendo vinavyoendelea Palestina na kwamba vitendo
hivyo vinakwenda kinyume na misingi na haki za kibinadamu.
Ameongeza
kuwa vitendo vinavyoendelea Palestina hivi sasa vinapingana na misingi
ya dini kuu duniani ikiwemo dini ya Kiislamu, hivyo kwa tamko hilo
BAKWATA linaitaka Jumuiya ya Kimataifa kuchukua hatua stahiki kusitisha
udhalimu huo usiokubalika.
"Aidha BAKWATA inawataka Waislamu wote
Tanzania kuitumia Swala ya Ijumaa kusoma dua maalum kuliombea taifa la
Palestina na kuendelea na dua za kunuti katika Swala zote tano kumuomba
Mungu alinusuru Taifa hilo na ulimwengu kwa ujumla dhidi ya balaa hili
kubwa na mabalaa mengine yote ulimwenguni,"amesema Muft wa Tanzania.
Akisoma
tamko hilo ,amesema " Mwenyezi Mungu tunakuomba uufanye ulimwengu uione
batili katika vazi lake la batili na uwaruzuku kuiepuka na utuoneshe
haki katika vazo lake la haki na uturuzuku kuitafuta na kuitetea."
Home
HABARI
BAKWATA YALAANI MAUAJI YANAYOENDEA PALESTINA, AOMBA WAISLAMU WOTE NCHINI KUTUMIA SWALA YA IJUMAA KUOMBA DUA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...