Benki ya Equity (T) leo imekabidhi mchango wa Shilingi milioni 10 kwa Bodi ya Usajili wa Makandarasi nchini (CRB), ili kufanikisha Mikutano ya Mashauri ya Wadau wa Sekta ya Ujenzi  nchini mwaka 2021.

 Pichani Waziri wa Ujenzi Mh. Eng. Dr. Leonard Chamuhiro akipokea mfano wa hundi kutoka kwa Mkuu wa Masoko wa Benki ya Equity(T) Godwin Semunyu. Wengine ni Mwenyekiti wa Bodi ya Makandarasi (CRB) Mhandisi Consolata Ngimba na viongozi wa taasisi hizo.

Mkuu wa Kitengo cha Biashara wa Benki ya Equity (T) Isabella Maganga, Akizungumza katika maonesho ya  sekta ya ujenzi leo jijini Dar es Salaam... amesema kama benki watasimama katika nafasi ya kuendelea kuongeza fursa ya upatikanaji wa huduma za kifedha ili kuendelea kuwawezesha wakandarasi kutekeleza miradi mbalimbali.

Amesema Benki ya Tanzania, inajivunia ubunifu ambao kwao ni kipaumbele na wataendelea kutengeneza huduma na bidhaa ambazo zitaweza kumudu uwezo wa kila mwananchi na wafanyabiashara na kwa kiwango kinachoridhisha.

Aidha amesema kuwa wataendelea kuunga mkono jitihada za Serikali kwa kuhakikisha miundombinu inaendelea kuboreka.

"Equity Bank tunasimamia dira na miongozo kwa kusikiliza na kujali wateja na huo ndio msimamo na utekelezaji wa benki yetu kwa wananchi." Amesema.


Akizugumza baada ya kukabidhi mfano wa hundi hiyo kwa Mheshimiwa Waziri Chamuhiro, Mkuu wa Masoko wa Benki ya Equity Godwin Semunyu amesema kuwa Benki ya Equity ni mdau mkubwa wa sekta ya ujenzi nchini hivyo imeona umuhimu wa kudhamini mkutano huo ili kuwakutanisha wadau wote  wa sekta hiyo kwa lengo la kubadilishana uzoefu na hivyo kuongeza tija.

 “Equity Bank imejipanga kuendelea kutoa huduma nafuu za kifedha kwa wakandarasi  wa ndani ili kuwaongezea mitaji  na hivyo kuwapa uwezo wa kushindana sokoni. Nichukue fursa hii kuwakaribisha wakandarasi wote nchini kutembelea matawi yetu ya Benki ya Equity ili wafurahie huduma bora na nafuu zaidi sokoni” alisema.

Maofisa wa Benki ya Equity

Waziri wa Ujenzi Mh. Eng. Dr. Leonard Chamuhiro akisaini kitabu cha wageni katika banda la Benki ya Equity katika mkutano huo. Kushoto ni Innocent Ndika Meneja Mwandamizi wa Mikopo wa Benki ya Equity.

Benki ya Equity pia imeandaa sehemu maalum katika jengo la Daimond Jubilee ambapo mkutano huo unafanyika, ili kutoa maelezo ya bidhaa zake kwa washiriki wa mkutano huo. 
















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...