Kampuni ya Meridian Bet yatoa  msaada wa vifaa vya michezo vilivyotolewa na kampuni ya kubashiri  matokeo ya Meridian Bet umeipa mzuka timu ya Lenster senior  league (LCL) wa kushinda ubingwa tena wa Ligi Kuu ya walemavu itakayoanza Juni mwaka huu.

Timu hiyo yenye wachezaji saba wa timu ya taifa imekabidhiwa msaada wa jezi, vikinga ugoko, njumu, mipira na soksi vilivyotolewa na Meridian Bet.

Meneja wa Meridian Bet, Ernest John  na Meneja Mwendashaji Mkuu  Tanzania, Corrie Borman walikabidhi msaada huo katika hafla fupi iliyofanyika makao makuu ya Meridian Bet na kueleza kuwa ni muendelezo wa kampuni yao kusaidia jamii yenye uhitaji nchini.

Nahodha wa LCL, Alphan Athuman aliyeambatana na wachezaji wengine na uongozi wa timu amesema msaada huo ni chachu kwao kufanya vizuri na kuuahidi uongozi wa Meridian Bet kurejea na kombe mwishoni mwa msimu baadae mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...