Na  Mwandishi  Wetu , Zanzibar
KAMPUNI ya Lavy Beauty Limited inayoongozwa  na Mkurugenzi wake  Flaviana Matata  imetoa   taulo za kike kwa wasichana 270 ambao ni wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Kiembe  Samaki iliyopo Maeneo ya Mazizini  Kisiwani Zanzibar.

Pia zawadi kama hizo zimetolewa  na Lavy Jijini Dodoma  kwa wasichana 480 ikiwa ni Katika kuadhimisha  siku ya  Hedhi Duniani.
Flaviana  alitoa zawadi hizo leo shuleni hapa aliongeza  kwa kuwahi anaiomba Serikali iwaondolee kodi kubwa ambayo wanalipa kwa sababu bidhaa ya taulo hizo za kike ni bidhaa isiyokuwa na faida pia ni muhimu kwa matumizi ya mtoto wa kike na wanawake kwa ujumla.
  
Sisi tunaingia gharama katika kutengeneza taulo zenye ubora hivyo nashauri waweke mpango wa kuzinunua na kugawa bure mashuleni.
 
Meneja wa Marie Stopped  Zanzibar David Mbange aliongeza kwa kusema kuwa kuwa siku ya hedhi duniani huadhimishwa kila ifikapo Mei 28 Mei kila mwaka  "Siku hii ina lengo la
kuwakutanisha wadau mbalimbali kwa dhumuni la kuongeza uelewa kuhusu masuala ya
hedhi na kuhamasisha upatikanaji maji safi , taulo(visodo) kwa wasichana na wanawake
hasa wale walio katika mazingira magumu. 

Mwalimu  Mkuu wa Shule ya Sekondari Kiembe Samaki Mussa Abdi Khamis amesema kuwa amefurahishwa na ujio wa Lavy na kutoa zawadi kwa wanfunzi wote wa kike na kiume.
Alisema kuwa hii Elimu wazazi wengi hawana muda wa kuwaelewesha vijana wao kwa uwazi huku akisisitiza kuwa mazingira ya hapa shuleni  kwake ni mazuri na rafiki kwani Kuna patikana maji  pia wanna kisima na Kuna waalimuwanaotoa ushauri nasaha.

Pia Lavy Limited Company tangu imeanzishwa inatoa taulo za kike kwa wasichana 2993 bure nchi nzima. 

Zawadi hizo za vitaulo zimetolewa katika mikoa mbalimbali ikiwa ni katika kuadhimisha Siku ya Hedhi Duniani.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...