Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam ambae kwa Sasa ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani Mhe. Abubakar Kunenge leo May 19 amekabidhi ofisi kwa Mkuu Mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makala ambapo amewashukuru Watumishi wote wa Mkoa huo kwa ushirikiano mkubwa waliompatia wakati wa uongozi wake.

RC Kunenge amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa Imani kubwa aliyomuonyesha kwa kumteua kuongoza Mkoa wa Pwani.

Aidha RC Kunenge amesema ushirikiano wa kazi baina yake na Watumishi wote wa Mkoa viliwezesha kupatikana kwa mafanikio makubwa ambapo ametoa wito kwa Watumishi hao kuendelea kumpa ushirikiano huohuo Mkuu wa Mkoa Mpya ili aweze kutimiza maono ya Rais Samia Katika Mkoa huo.

Kwa upande wake Mkuu mpya wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makala amempongeza RC Kunenge kwa kazi kubwa na nzuri aliyoifanya Katika Mkoa huo na kueleza kuwa anaamini uwezo alioonyesha Dar es salaam ataupeleka Mkoa wa Pwani.

Makabidhiano ya ofisi yamefanyika mbele ya Viongozi wa Mkoa huo akiwemo Katibu Tawala wa Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wastaki Meya, Viongozi wa Usalama, Makatibu Tawala wa Wilaya na Wakuu wa Idara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...