Na Mwandishi wetu, Babati
MAONYESHO
ya 16 ya kanda ya kaskazini ya Shirika la kuhudumia viwanda vidogo
nchini SIDO, yanatarajia kufanyika kwa siku tano Mjini Babati Mkoani
Manyara huku yakihusisha nchi nne za Afrika Mashariki.
Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Babati, Mkuu wa Mkoa wa
Manyara, Charles Makongoro Nyerere amesema maonyesho hayo yatakayoanza
Mei 27 hadi Mei 31 mwaka huu, yatahusisha pia nchi za Uganda, Kenya,
Rwanda na Burundi.
Makongoro
amesema maonyesho hayo yatafunguliwa rasmi Mei 28 na Waziri wa Viwanda
na Biashara Kitila Mkumbo na kufungwa naye mkuu huyo wa mkoa Mei 31.
"Pia
taasisi mbalimbali nchini zinazohudumia wajasiriamali zitakuwepo
wakiwemo TRA, TBS, Brella, NMB, CRDB, NBC, TPB na Azania benki," amesema
Makongoro.
Meneja wa
Sido mkoani Manyara, Abel Mapunda amesema kauli mbiu ya maonyesho hayo
ni maendeleo ya viwanda nuru ya mafanikio kiuchumi.
Mapunda
amesema kupitia maonyesho hayo wananchi watapata fursa ya kujifunza
shughuli zinazofanywa na taasisi zinazohudumia wajasiriamali.
"Maonyesho
haya siyo kwa ajili ya wajasiriamali pekee hata wananchi wanakaribishwa
kutembelea mabanda katika uwanja wa Kwaraa ili kujionea bidhaa na
teknolojia mbalimbali zinazotengenezwa Tanzania," amesema Mapunda.
Meneja wa shirika la kuhudumia viwanda vidogo nchini (SIDO) Mkoa wa Manyara, Abel Mapunda, akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Manyara Charles Makongoro Nyerere (katikati) juu ya maonyesho ya 16 ya Kanda ya kaskazini yatakayofanyika Mjini Babati, kulia ni Ofisa habari wa Mkoa huo, Haji Msovu.
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Charles Makongoro Nyerere,
akizungumzia maonyesho ya 16 ya shirika la kuhudumia viwanda vidogo
(SIDO) ya kanda ya kaskazini, yatakayofanyika kwa siku tano mjini
Babati, kushoto ni Meneja wa SIDO wa Mkoa huo Abel Mapunda.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...