Na Mwamvua Mwinyi, Pwani

MKUU wa Mkoa wa Pwani,Aboubakar Kunenge,, ametoa onyo  kwa watendaji wa Bodi ya Maghala na Wakala wa Vipimo ,mkoani humo, kushindwa kupima mizani zilizopo kwenye maghala ya vyama vya Msingi zinazotumika kupokelea Ufuta na  kushindwa kusimamia maandalizi ya Maghala Makuu, hali inayosababisha kero na kusuasua kwa zao hilo.

Alitoa onyo hilo,wakati akiendesha Mkutano wa Wadau wa Ufuta,Ikwiriri Wilayani Rufiji.

Kunenge alikerwa na watendaji hao wa Serikali kusubiri kuitwa na  Wakulima badala ya kuwafuata na kutoa huduma. 

Alieleza ,hahitaji kuona ubabaishaji,kwani hatosita kuwaondoa kwa kushindwa kusimamia wajibu wao kikamilifu.

Aidha Kunenge alitoa muda wa Siku tatu kwa watendaji hao ,kuhakisha kuwa wanakamilisha maandalizi ya Maghala  Makuu na Upimaji wa Mizani kwenye maghala ya Msingi.

 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...