Uongozi wa Chama cha Skauti Tanzania umetakiwa kuwafinyanga vijana kiuzalendo ili kuwajenga maadili mema yatakayowawezesha kupiga vita vitendo viovu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla alieleza hayo alipokutana kwa mazungumzo na uongozi wa Chama hicho uliofika Ofisini kwake Vuga jijini Zanzibar.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alieleza kuwa mafunzo ya skauti ni eneo muhimu kwa maslahi ya taifa kutokana na mchango wake mkubwa katika kuwajengea maadli mema vijana sambamba na kuwapatia elimu ya ubunifu.
Aidha amesema kuna haja kwa uongozi wa Skauti Tanzania kuwafunza vijana namna bora ya kuweza kutambua ubaya na kupinga rushwa, ubadhirifu pamoja na uhujumu wa uchumi.
Akigusia suala la mashirikiano Mhe. Hemed ameuhakikishia uongozi huo kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar itatoa ushirikiano wake, katika kuhakikisha mchango wa chama hicho unatambulika Nchini.
“Jamii lazima itambue kwamba kazi ya kuwalea vijana si ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali na Chama hicho pekee, bali ni jukumu la jamii kwa ujumla.
Nae Makamu mwenyekiti wa chama hicho ambae pia ni waziri wa elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mhe. Simai Mohamed Said alisema Wizara anayoisimamia itahakikisha wanawapa mashirikiano ya uongozi wa Skauti Tanzania kwa lengo la kusimamia utendaaji kwa vijana wa Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.
Pamoja na mjabo mengine Mhe. Simai alieleza kuwa Chama cha Skauti kwa upande wa Zanzibar kimeimarika vyema katika kusaidia malezi bora katika jamii.
Mapema akitoa taarifa kwa Makamu wa Pili wa Rais Mkuu wa Chama cha Skauti Tanzania Mwantum Bakari Mahiza alisema chama hicho kwa upande wa Zanzibar kina zaidi ya miaka 109 tangu kuanzishwa kwake ambapo kimekuwea kikipata mashirikiano mazuri kutoka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar.
Kiongozi huyo alimueleza Mhe. Hemed kuwa hivi sasa uongozi wa Skauti unajenga kambi ya kimaitaifa Makao Makuu ya Nchi Jijini Dodoma hivyo alitumia fursa hiyo kuiomba Serikali ya Mapinduiz ya Zanzibar kuwapatia eneo maalum kwa ajili ya kujenga chuo cha kutolea mafunzo kwa vijana.
Chama cha Skauti Nchini Tanzania kina
jukumu la kulea na kuwafunza nidhamu na maadili mema, ukakamavu kwa vijana wa
kitanzania kwa taasisi mbali mbali za SMT na SMZ.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...